Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dokta John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hatua anazochukua kukabiliana na Upotevu wa Mapato ya Serikali katika Sekta ya Madini

Hon. Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dokta John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hatua anazochukua kukabiliana na Upotevu wa Mapato ya Serikali katika Sekta ya Madini

MHE. CAPT. GEORGE H. MKUCHIKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa tena nafasi. Mimi leo nimefarijika sana katika Bunge hili. Watu wote waliochangia upande wa CCM na upande mwingine hakuna aliyesema Rais kakosea. Hakuna aliyesema Rais kakosea, mwingine anasema hapana tunashangilia mapema mpira, tusubiri mwishoni. Mimi ninavyofahamu mpira unashezwa dakika 90, filimbi ikipigwa tu mwenye timu yake anashangilia hangoji dakika ya mwisho. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kusema kwa kifupi sana, ndugu yangu pale Mheshimiwa King ameunga mkono hoja tunashukuru, Mheshimiwa Mchengerwa ameunga mkono hoja tunashukuru, ndugu yangu Mheshimiwa Mtolea pale ndiyo yule kasema kwa nini tunapongezana bado safari ni ndefu (encouragement), watu wote wa Tanzania wanajua kwamba Rais anafanya kazi ngumu ili aendelee kuifanya ile kazi nzuri anahitaji kutiwa moyo, ndiyo hiki tunachokifanya hapa. Hata hivyo, nampongeza ndugu yangu Mheshimiwa Mtolea, wala hajasema Rais kakosea kuunda wala hajasema, ndiyo nilichompenda hicho. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia anasema tuongeze nguvu za kuzuia dhahabu. Kwa upande mwingine ukilinganisha lugha yake hiyo ni kama vile yupo pamoja na Rais, hivi wenzangu mnaonaje? (Makofi/Vigelegele)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndugu Mheshimiwa Hasunga ameunga mkono hoja, lakini hili suala la mikataba mimi nilisikiliza juzi Rais wakati anapoongea, alisema yale mambo ya kisheria, pale ambapo mikataba haikukaa sawa, pale ambapo sheria haikukaa vizuri, Serikali itatuletea hapa Bungeni ili tuipitie na kurekebisha. Sasa naomba usitie unga kupika ugali kabla maji hayajachemka. Ukitia mapema utapata uji badala ya ugali. Tusubiri muda ukifika hiyo kazi tutaifanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndugu yangu Mheshimiwa Kangi Lugola ameunga mkono, ndugu yangu Mheshimiwa Tundu Lissu pale alikuwa anacheka maana yeye pamoja na lugha yote ya ukali, hakuna Mheshimiwa Tundu Lissu aliposema napinga Rais kuunda Tume, mmemsikia anasema hivyo? Tuko naye pamoja katika hili. (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, unajua Bunge moja hapa aliwahi kuja Spika wa Bunge la Kenya anaitwa Ole Kaparo, akasema kwamba, katika nchi zingine vipo vyama vinaitwa Chama Pinga. Chama Pinga maana yake yeye hata ukimwambia mbili jumlisha mbili jawabu nne atakwambia hapana tano. Sasa sifikiri kama ndugu yangu Mheshimiwa Tundu Lissu amefika huko kwenye hatua ya kusema mbili jumlisha mbili saba. Kwa hiyo, nasema nimemsikiliza sana ndugu yangu Mheshimiwa Lissu yeye ni mzalendo na jana kwa mfano hata wenzetu upande wa Upinzani walisema,. tulikuwa tukipiga kelele hamkutusikia, hamkutusikia, sasa tumekusikieni leo, si mseme basi Alhamdulillah mmetusikia. (Makofi/Vigelegele)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lile la kuwasifu Marais waliotangulia nadhani Mkuu wa Shughuli za Serikali Bungeni kasema, sisi ni Bunge la mwaka 2015-2020 tunashughulika na mambo yaliyomo ndani ya kipindi chetu. Wale Marais waliotangulia walianza Magufuli anaendeleza pale walipoachia wenzake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, kama nilivyosema sitaki kupoteza muda, hili Azimio limepokelewa vizuri, pande zote mbili wamelipamba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa hoja.