Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dokta John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hatua anazochukua kukabiliana na Upotevu wa Mapato ya Serikali katika Sekta ya Madini

Hon. Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kumpongeza Mheshimiwa Dokta John Pombe Joseph Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa hatua anazochukua kukabiliana na Upotevu wa Mapato ya Serikali katika Sekta ya Madini

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru nami kwa kunipa nafasi ya kuchangia Azimio hili japo kwa uchache kwa hizi dakika chache ambazo umetugawia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini napatwa na mshituko mkubwa kuona ni kwa nini tunaanza kupongezana mwanzo wa safari, tumezoea kupongezana pale kazi inapokamilika. Kuundwa kwa Tume hakujaanza leo, hakujaanza jana, nikiwa niko mwanafunzi sekondari miaka ya 1997-1998 tulikuwa tunaona Mheshimiwa Benjamin Mkapa aliunda Tume zikafanya kazi, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete aliunda Tume zikafanya kazi, hawa wote tungeanza kuwapongeza pale tu walipounda Tume mwanzoni kabla ya kazi kukamilika tungekuwa tuko wapi? Lazima tuache kazi ifanyike, madini bado yanaibiwa kwa kiasi kikubwa migodini leo tukianza kupongeza kuzuia makinikia peke yake tunakuwa tunakosea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye maisha kuna vitu viwili vya kuchangua ama uchague kuwa mtendaji au uchague kuwa mshangiliaji. Bunge tunaamua kuwa washangiliaji, hili ni jambo la kusikitisha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliamua kubeza hoja nzito zinazohusu kuyalinda madini yetu wakati muafaka, akina Peter Serukamba hawa walipiga kelele hapa, Hamisi Kigwangalla huyu alikamatwa na kuteswa huko kwa sababu ya madini, John Mnyika, Tundu Lissu, Zitto Kabwe walizungumza mambo haya na tuliamua kuwabeza. Leo kwa sababu imepigwa ngoma na tunayempenda tumeamua kuishangilia, tunaishingilia kwa sauti nzito nzito. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulitendee haki Bunge hili, tunapoingia hapa Bungeni tuvae viatu vya Kibunge tuenee ili tuishauri Serikali na tusijigeuze kuwa washangiliaji tu wa Serikali. Inasikitisha sana, tukilichukulia jambo hili rahisi rahisi kama vile limekwisha na kilichofanyika ndiyo kinatosha tunapoteza rasilimali za nchi hii. Kama Bunge tukae na tuone kwamba kama Rais ana nia nzuri kiasi hiki na sisi Bunge tumsaidie kwa ku-pressurize sheria zote za mikataba tuzifanyie amendments hapa haraka iwezekanavyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mapande ya dhahabu bado yanaendelea kuondoka na kwa sababu tayari hizi indicator za kuzuia zimeanza, tukichukua muda mrefu kabla hatujayazuia haya, watu wataongeza speed ya kuziiba kwa sababu wanajua mwisho wao unakaribia. Tuongeze nguvu ya kuzuia rasilimali zetu ziache kuibiwa, kupongezana ni jambo dogo sana, tunaweza kupongezana wakati wowote na wala siyo lazima tukapongezana kwenye Bunge, tunaweza kupongezana kwenye mabaraza ya kahawa, tunaweza kupongezana… (Makofi/Vigelegele)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)