Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipatia nafasi, naanza kwa kuunga mkono hoja iliyoletwa na Kamati zote mbili.

Mheshimiwa Naibu Spika, dakika mbili nyingi sana kwangu kwa sababu nategemea kutoa ufafanuzi kwenye eneo moja tu nalo liko ukurasa wa 38 ni kuhusiana na ubovu wa barabara za mipakani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo sisi kama Taifa tumekuwa tukiweka vipaumbele kwa barabara ambazo zinaunganisha Mikoa, lakini pia kuna umuhimu mkubwa sana kwa barabara za mipakani na hasa barabara yetu ya kwenda Uganda kule kwa kupitia chombo chetu cha TARURA tutahakikisha kama Serikali ukarabati unafanyika ili barabara hii iwe nzuri iweze kusaidia katika shughuli nzima za kulinda mipaka yetu, ahsante sana.