Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Dr. Harrison George Mwakyembe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru na mimi kwa kunipa nafasi niweze kuchangia katika hoja zilizoko mbele yetu hapa.

Mheshimiwa Naibu Spika, wiki hii kutakuwa na matukio mawili muhimu ya sehemu ya mahusiano ya kimataifa tuna mechi mbili za mpira kati ya Timu za Tanzania na timu kutoka Seychelles na kutoka Djibouti. Sasa Mheshimiwa sijui kuna kitu nafikiri kiliongelewa hapa maana kwenye simu yangu nakuta kila mtu ananiuliza kwamba kuna tatizo na tumefanya upendeleo kwa timu ya kimataifa kufanya mazoezi kwenye uwanja wa Taifa, lakini timu ya hapa Tanzania haijapewa nafasi kufanya.

Ningeomba nitumie fursa hii kwa sababu ni mambo ya foreign affairs haya niweze kuitolea ufafanuzi kwa kifupi sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, wote mnajua tu kwamba tumefanaya ukarabati mkubwa wa kiwanja chetu uwanja wetu wa Taifa mwaka huu majuzi tu, tumekamilisha baada kiwanja hicho kutuhudumia kwa zaidi ya miaka 10 na ukarabati tulioufanya vilevile nyasi tulizoweka pale zinategemea zitatuhudumia kwa zaidi ya miaka 10 na ili ziweze kufika miaka 10 kuna masharti yake, haturuhusiwi hicho kiwanja kukitumikisha kikabeba michezo zaidi ya mitatu kwa wiki moja, ukifanya hivyo unaingiza uswahili na hata ikiharibika mapema huwezi hata kwenda kudai mtu aliye ku-gurantee kwamba kitaa miaka 10.

Kwa hiyo, wiki hii tuna mechi mbili muhimu; kesho wanaingia Young Africans wanashindana na timu kutoka Seychelles na kesho kutwa wanaingia Simba na timu kutoka Djibouti. (Makofi)

Kanuni za kimataifa zinataka timu ngeni hiyo ya kimataifa lazima ifanye mazoezi kwenye hicho kiwanja kitakachofanyiwa mechi na vilevile FIFA inatambua kwamba hiki kiwanja ni cha timu ya hapa nchini kwa hiyo uwanja wa Taifa ni uwanja wa Yanga, uwanja wa Simba unategemewa ujue uwanja wako sasa wale wengine hawajajua ndio maana wanaopewa priority kuweza kufanya mazoezi pale.

Mheshimiwa Naibu Spika, tayari tuna mechi mbili na kwa sababu tunaruhusu hawa wageni kufanya mazoezi pale ambao ni lazima kwa hiyo tutakuwa tumekiuka tayari tuna michezo minne ndani ya wiki moja. Na usisahau wiki hii hii Azam na Simba wamecheza uwanja huo huo, kwa hiyo mara tano, uswahili umeanza kuingia katika uwanja wetu wa Taifa.

Mimi nashukuru kwa haya maneno niliyoyapata nadhani kuna vijana wangu pale wanahitaji kwa kweli wadhibitiwe, utaruhusuje mechi tano katika uwanja huo ambao utarudia mara tatu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nilitaka kufafanua tu kwamba ni haki ya wageni kupewa nafasi na sisi tuweze kutumia viwanja vyetu na naniombe nitoe rai na wito kwa wapenda mpira hapa, timu ya Yanga ina umri wa miaka 83 timu ya Simba ina umri wa miaka 82 timu zetu sasa zifike muda nazo zijenge viwanja vyake.