Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Naibu Naibu Naibu Spika, naomba nichangie hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, hali ya ulinzi na usalama wa raia na mali zao; inasikitisha sana kushuhudia matukio yanayohatarisha maisha ya raia na mali zao na kusababisha hofu kubwa miongoni mwa wananchi. Mathalani, kumekuwa na kupotea kwa wananchi wengi katika maeneo mbalimbali kama vile kupotea kwa Ben Saanane na wengine. Naiomba Serikali ichukue hatua za haraka kuhakikisha inadhibiti matukio haya.

Mheshimiwa Naibu Naibu Spika, ulinzi na usalama wa Wabunge; kwa kweli inasikitisha sana kwa kuwa Wabunge hawana ulinzi wowote na hata maeneo wanayoishi hayana ulinzi wowote. Naomba Serikali ijifunze kutoka nchi nyingine namna Wabunge wanavyolindwa wao na mali zao.

Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania inasikitisha kuona Wabunge wanajilinda wenyewe na hii imehatarisha maisha ya Wabunge na hata kupelekea Wabunge hao kuvamiwa na kupigwa risasi mfano, Mheshimiwa Tundu Lissu, aliyepigwa risasi 38 hapo mwaka jana. Naiomba Serikali kuleta marekebisho ya Sheria ili kiingie kipengele cha kuweka walinzi kwa ajili ya Wabunge, siyo hapa Bungeni tu bali hata maeneo wanayoishi Wabunge.

Mheshimiwa Naibu Naibu Spika, kukamatwa Wabunge kwenye maeneo ya Bunge, kumekuwa na kamata kamata Wabunge kwenye maeneo ya Bunge. Huu ni udhalilishaji wa Wabunge, maana ya kinga za Bunge ni nini? Naiomba Serikali ilete marekebisho ya sheria kuheshimu maeneo ya Bunge ambapo Wabunge wana kinga pia askari wawe na heshima kwa Wabunge na hasa wawapo kwenye Majimbo yao, maana askari wanawadhalilisha Wabunge. Mfano, mnamo tarehe 16 Novemba, 2017, Mbunge wa Viti Maalum alidhalilishwa na askari kule Kilolo Kata ya Kimala.

Mheshimiwa Naibu Naibu Spika, mrundikano wa mahabusu na wafungwa; katika magereza mengi hapa nchini kuna mrundikano wa mahabusu ambao wakati mwingine hawana kesi yoyote, bali wanajaza magereza, mfano, Gereza la Njombe Mjini kuna mrundikano wa mahabusu, naomba kuishauri Serikali mahabusu ambao hawana kesi, kesi zao ziharakishwe kusikilizwa ili kuondokana na mrundikano wa wafungwa.

Mheshimiwa Naibu Naibu Spika, naomba kuwasilisha.