Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii nami niweze kuchangia kwenye taarifa hizi mbili ambazo zimewasilishwa na Wenyeviti. Napenda niwashukuru Wenyeviti wamewasilisha taarifa zao hizi kwa weledi na umakini mkubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Bunge la Tisa tulifanyiwa semina na watu wa Usalama wa Taifa, kuna mfano mmoja walileta wale watu wa Usalama wa Taifa, Kiongozi mmoja wa nchi hapa Tanzania amepelekewa zawadi ya Qurani, kitabu cha Mungu cha Qurani kapelekewa. Kwa kuwa ni Kiongozi mkubwa watu wa katikati waliingilia kuifungua kwanza ile Qurani, kumbe lilikuwa ni bomu tulioneshwa hapo. Sasa juzi Mheshimiwa Spika Mbunge mwenzetu amepigwa risasi moja.

Mheshimiwa Naibu Spika, mbili, Jenerali mmoja Mstaafu wa Jeshi kapigwa risasi hicho ni kiashiria kwamba silaha zipo ‘bwelele’ nchini kwetu. Zipo bwelele kwa sababu tuna changamoto nyingi sana, hali ya majirani zetu Sudan, Somalia, Congo vita iliyoko huko inafanya na mipaka yetu ipo porous, silaha nyingi zipo nchini hapa sana; pia utandawazi uliopo duniani; tatu, kukosa ajira kwa vijana wetu ambao wanarubuniwa na watu wanaopigana vita huko na kuwafundisha ugaidi. Hizi ni changamoto ambazo zinaonesha kwamba usalama wa Viongozi hapa Tanzania is an issue of the sense kwa sasa.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakuomba sana Bunge lichukue hatua madhubuti kuhakikisha Wabunge, Wabunge ambao ni baadhi ya Viongozi, Wabunge ambao hapa Bungeni tunaongea mambo ambayo yanawagusa wengine huko nje ambao wana uwezo wao kifedha na kigaidi, wawekewe usalama. Usalama hapa Dodoma kwenye makazi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa nasema kwamba, naliomba Bunge lichukue hatua madhubuti sana kuhakikisha usalama wa Wabunge kwa sababu ni Viongozi. Kwa sababu mambo ambayo wanaongea Wabunge hapa ndani yanawagusa watu wengine huko nje ambao wana uwezo wa kifedha na uwezo wa kigaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, Bunge la Kumi lilianzisha mchakato wa kuwa na Kijiji cha Wabunge hapa, naomba wazo hilo liendelee, nyumba zijengwe Wabunge wote wake sehemu moja ili waweze kupatiwa ulinzi. Huko kwenye Majimbo yetu Wabunge wapewe ulinzi kama anavyopewa ulinzi Mkuu wa Wilaya.

Mheshimiwa Naibu Spika, nne, Wabunge magari yao yatambuliwe, yawe na namba ambazo zipo sawasawa na zinajulikana kwamba huyu ni Mbunge wa Lupa, namba yake ipo pale, vinginevyo Wabunge wengi wataanza kupigwa risasi, Viongozi wengi wataendelea kupigwa risasi. Usalama wa Wabunge, usalama wa Viongozi wote nchini Tanzania sasa hivi ni issue ambayo ipo top of the agenda.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana na naunga mkono hoja.