Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niwapongeza kwa kazi nzuri Kamati iliyofanya. Naomba nichangie kwanza kwa kuliomba Bunge liangalie namna ya kuratibu kazi za Kamati ili Wabunge wapate fursa ya kuchangia wanaotoka Kamati zingine ili taarifa na maazimio ya Kamati kuzishauri Serikali namna ya kutatua changamoto mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza katika shughuli za Kamati nichangie suala la afya. Niipongeze Serikali kwa kuboresha na kufanya vituo vya afya ambavyo vitakidhi haja ya huduma za afya katika ngazi ya kata. Nashauri Wilaya zisizo na hospitali kwa sasa wasikimbilie kwenye hospitali bali waboreshe huduma za afya ya msingi katika kata mbalimbali itaharakisha huduma kuwa karibu na jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Serikali ikubali sehemu ambapo Kata, Wilaya au Kijiji wana ramani zao za majengo ambayo yanakidhi mahitaji bila kuondoa ubora wa majengo waruhusiwe kuwa na ramani zao (different design in architecture).

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali iangalie gharama za vifaa tiba na madawa yanayosambazwa na MSD kama tunafanya bulk procurement mbona bado kwa watu binafsi bei ni karibu sawa au wakati mwingine ni bei ya chini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba suala la non communicable diseases (magonjwa yasiyoambukizwa) litiliwe mkazo na kupewa umuhimu kama Kamati ilivyoshauri. Elimu juu ya magonjwa hayo itolewe kwa kasi zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la lishe bora, Serikali iondoe kodi kwenye virutubisho vya kuchanganya kwenye unga na mafuta vya kupitia. Leo hii ni kwa taasisi za Serikali tunazopata huo msamaha na Serikali haina hata kiwanda kimoja, suala la lishe bora hatutafikia kwa tamaa za kupata kodi. Wenye viwanda wameacha kuweka hivyo virutubisho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunashauri Serikali iangalie namna ya kuongeza bajeti ya COSTECH; bajeti ya utafiti na maendeleo. Tupange asilimia moja ya bajeti au bilioni 120.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Serikali iangalie kwa bajeti hii kuchangia kituo cha kutengeneza mafuta ya wenye ulemavu wa albino pale KCMC. Kitengo cha ngozi tuwekeze katika dawa za asili (homeopathy).

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika elimu nashauri tuangalie namna ya kurudisha asilimia mbili ya SDL inayoenda Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu kwenda VETA. Bodi itafutiwe chanzo kingine. VETA ipate haki yake ya asilimia nne. Pia tubadilishe mitaala ya kuwa ya mfumo wa IT, kutumia kompyuta. Leo hii hawa vijana tunaowafundisha kwa teknolojia ya zamani watakosa ajira, leo mfano haya magari ya kisasa lazima ujue kutumia kompyuta, huwezi kurekebisha bila teknolojia, hata fundi umeme wa nyumba, taa na vifaa vingi vinatumia sensors, kama hawajui IT (masuala ya kompyuta) namna ya ku-programme elimu yao haitahitajika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuwekeze kwenye utafiti na maendeleo, COSTECH tupange angalau bilioni 120 kwa mwaka; asilimia moja ya bajeti nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Vyuo Vikuu Maalum kama SUA, virudishwe chini ya Wizara husika ili vipate huduma za karibu zaidi. Chini ya Wizara ya Elimu haviwezi kupata kipaumbele na Wizara kwa haki inatenga bajeti sawa kwa wote. Chuo cha Nelson Mandela kingeenda Wizara ya TAMISEMI pamoja na VETA zote, vyuo vya afya viende Wizara ya Afya. Aidha, vyuo vikuu viwe specialized na hata suala la field katika masomo yao lingepata unafuu.