Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni kuhusu uwasilishaji wa Sheria Ndogo Bungeni; kwa kuwa kuna sheria ndogo ndogo ambazo zina dosari, naishauri Serikali kuleta hapa Bungeni na kufanya marekebisho hapa Bungeni kwa mfano; Sheria ya Vyombo vya Usafiri ambayo inatumika kwa vyombo vyote vya usafiri kuanzia bodaboda hadi magari makubwa. Kama ni kulipa faini wote wanalipa sawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Sheria ya Ndoa inayoruhusu watoto chini ya miaka 18 kuolewa ibadilishwe na kuweka umri wa kuolewa uwe miaka 18 na siyo chini yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia naiomba Serikali ilete marekebisho ya Sheria ya Ardhi ambayo itawaruhusu wanawake kumiliki ardhi kuliko ilivyo sasa kwamba ni wanaume tu wanamiliki ardhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha