Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nipongeze na kuunga mkono hoja iliyopo mezani juu ya Taarifa ya Kamati ya Sheria Ndogo iliyowasilishwa vizuri na Mwenyekiti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Bunge liwe macho juu ya sheria zozote inapotokea zinakinzana na Katiba ya nchi au inapokinzana na uhalisia wakati wa utekelezaji nikimaanisha sheria inapokuwa haina maslahi kwa jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningeshauri sheria ya umri wa mtoto wa kike kuolewa itoe uangalizi wa sheria hii kwani watoto wa kike sasa hivi wanabalehe mapema, hivyo, naishauri Serikali iangalie kwani sasa hivi ina mchanganyiko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali kuleta muswada wa sheria kuhusu mwanamke kuwa na haki ya kumiliki ardhi ya familia, sio kama ilivyo sasa ambapo haiko hivyo.