Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja na mapitio ya hoja za Kamati za Sheria Ndogo zinazopitishwa na Halmashauri zetu nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ziko changamoto chache ambazo kimsingi zinasumbua walipa kodi na kupitia TAMISEMI, kwanza ni ushuru wa maegesho za Halmashauri ya Mji lengo ni kutoza faini kwa maegesho holela na wamiliki wa vyombo vya moto wamekuwa wakitozwa faini hizo shilingi 50,000 na mmiliki akishindwa kulipa anapelekwa mahakamani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, faini hizi kupitia sheria hizi ndogo usimamizi wa pesa hizi TAMISEMI (kupitia Wizara ya Katiba na Sheria). Je, Serikali haioni kuwa sheria hii ni kandamizi kwa sababu Halmashauri nyingi hazijatenga maeneo ya kutosha ya maegesho hayo hususani mijini? Na je, wananchi wana uelewa kiasi gani kuhusu faini hizi na je, hamuoni kwamba ni Serikali yenyewe ilitakiwa itengeneze mazingira ya maegesho makubwa ili uonevu huu usiendelee?

Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria zilizopitishwa na Halmashauri zetu kupitia makanyagio ya ng’ombe katika minada yetu nchini ushuru huu kwa wafugaji unawakandamiza sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfugaji anasafiri kutoka Tarafa moja kwenda nyingine umbali wa kilometa 40 mfano kutoka Karema mpaka Mpanda Ndogo mfugaji anaende mnadani, anapoingia getini analipa ushuru auze/asiuze analipa ushuru na ng’ombe wanaposafirishwa kutoka katika minada katika mageti wanalipa tena.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria hii haiko sawasawa maana kuna ushuru mwingi kwa wafugaji na inawaumiza wafugaji. Serikali ilione hili ili angalau wafugaji hawa wawekewe mfumo wa kulipia mifugo yao kwa mara moja na sio ushuru wenye usumbufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushuru wa kutupa taka, sheria mama na sheria ndogo zote zinalenga kuisaidia jamii kuzifuata sheria hizi kupitia mamlaka zilizopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado nasisitiza kupitia sheria hii ni nzuri kwa maana ya kutunza mazingira kwa katika hali ya usafi. Je, Serikali imeweka mazingira gani kabla ya kutunga sheria hizi? Serikali ione haja ya kuhakikisha wananchi wanapata elimu ya kutosha na kupatiwa vifaa vya usafi halafu utekelezaji wa sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kupitia sheria hizi ndogo Serikali iangalie upya mazingira ya afya kwa shule za msingi ambazo hazijakidhi vigezo. Mfano sheria inasemaje kwa shule za msingi ambazo watoto wanatumia tundu moja la choo na ni shule za msingi za Serikali, ni kwa nini mazingira haya magumu yako wazi Halmashauri ipo? Sheria inasemaje?

Mheshimiwa Mwenyekiti, uwazi wa sheria na semina kwa Madiwani katika Halmashauri nchini, kwa kuwa Madiwani wengi hawana elimu ya kisheria na wao ndio watunga sheria katika Manispaa na hivyo kupitia kukosa weledi wa kisheria inapelekea Madiwani kutunga sheria kandamizi. Je, Serikali inasimamia vipi kuhusu semina kwa Madiwani wetu kuhusu masuala ya sheria?