Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Stella Ikupa Alex

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

AIBU WAZIRI, OFISI YA WZIRI MKUU, WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru, kwa ajili ya muda naomba niende haraka haraka nikiwapongeza Wenyeviti na Wajumbe wa Kamati zote mbili za Sheria Ndogo pamoja na Kamati ya Katiba na Sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba niongelee kidogo kuhusiana na hoja ya Kamati ya kutokuwa na mafungu ya moja kwa moja kwenye Ofisi ya Mheshimiwa Waziri Mkuu ya kibajeti kwa ajili ya maendeleo ya vijana pamoja na watu wenye ulemavu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba ikumbukwe kwamba masuala ya watu wenye ulemavu pamoja na vijana ni mtambuka, kwa maana kwamba yapo ambayo yanayoshughulikiwa moja kwa moja na Ofisi ya Waziri Mkuu, lakini pia yapo yanashughulikiwa na Ofisi ya Mheshimiwa Rais, TAMISEMI, na pia Wizara ya Afya pamoja na Wizara ya Elimu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na hilo Ofisi ya Waziri Mkuu sasa hivi inaendelea na zoezi la kukamilisha uundwaji wa Mfuko wa Taifa wa Watu Wenye Ulemavu. Mfuko huu utasaidia sana watu wenye ulemavu kwa kuwa mambo mengi ambayo yanahusu watu wenye ulemavu yatakuwa solved, ikiwa ikiwa ni pamoja na tafiti za watu wenye ulemavu, pia mambo ya elimu pamoja na mafunzo kwa watu wenye ulemavu, mambo pia ya ruzuku za vyama vya watu wenye ulemavu na mambo mengine ambayo yanahusu mambo ya ulemavu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ikumbukwe kwamba katika Ofisi ya Waziri Mkuu kuna Idara ya Maendeleo ya Vijana, idara hii ina mfuko wa vijana na mfuko huu unasaidia sana kwa habari ya mikopo ya vijana ambao wanafanya biashara mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukisema vijana ni pamoja na kundi la watu wenye ulemavu, kwa hiyo hii hoja ni ya msingi na kwa ufupi wake nimeitolea ufafanuzi kwa jinsi hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, haraka haraka tena kulikuwa na hoja kwamba Serikali itenge fedha kwa ajili ya Baraza la Ushauri la Watu Wenye Ulemavu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilihakikishie Bunge lako Tukufu kwamba Serikali inaendelea kutenga fedha kwa ajili ya Baraza la Ushauri la Watu Wenye Ulemavu na hivyo limeendelea kufanya vikao vyake vya kuishauri Serikali kama ambavyo Sheria Namba 9 ya mwaka 2010 ya Watu Wenye Ulemavu inavyoelekeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia kulikuwa kuna masuala ya utengwaji wa bajeti ya watu wenye ulemavu pamoja na vijana. Kama ambavyo nimeeleza hapa mwanzoni ni kwamba Serikali imeendelea kutenga fedha ingawa….(Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)