Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Suleiman Masoud Nchambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti nipo kwenye orodha ya kuchangia, samahani unajua, kwanza kabisa nataka niwafahamishe Waheshimiwa Wabunge wala msishangae, wajinga wameendelea kuwepo ili wafanye wenye akili waendelee. (Makofi).

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, baada ya kusema kauli hiyo ili kumrekebisha mwenzangu naomba sasa nichangie kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali hii inayosemwa haifuati utaratibu, sheria ama Katiba, jambo hili ni la kushangaza sana. Yapo mambo ya msingi ambayo Rais wa Awamu Tano ameyaainisha kama dira katika Taifa hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja mwaka huu na mwaka jana na awamu hii ya Rais John Pombe Magufuli ni awamu ya kazi. Mimi nashindwa kuelewa, mambo mengine ni ya kushangaza sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mzee wao, mshauri wao wa chama chao amekwenda Ikulu kumpongeza Rais kwa kazi nzuri anayoifanya. Kama Mzee Lowassa amekwenda Ikulu kumpongeza John Pombe Joseph Magufuli, jambo la kwanza ana ainisha bayana kuwa Katiba ya nchi hii inafuatwa ndiyo maana anampongeza, lakini ana hakika sheria za nchi hii zinafuatwa ndiyo maana anampongeza. Utekelezaji wa Ilani, kwa maana ya kuwasaidia wanyonge na maskini wa Taifa hili kazi hiyo inafanyika. (Makofi)

Msheshimiwa Mwenyekiti, maneno haya hata kanga yapo na mimi niwashukuru sana akina mama wana hekima na busara, maneno haya huwa wanayavaa katika kanga zao tena nyuma kwa chini kabisa, kwa hiyo ndiyo maneno anayoleta mheshimiwa hapa wala tusishangae.

Mheshimiwa Mwenyekiti…

T A A R I F A . . .
MHE. SULEIMAN M. NCHAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na naomba niendelee na michango yangu. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, taifa hili lilipokuwa limefika na kufikishwa na watu wachache waliokuwa wakishawishi miradi mizuri na mikubwa, mfano mradi wa reli, kwa kipindi kirefu Serikali ya Chama cha Mapinduzi, ilitaka kutekeleza miradi mikubwa lakini watu wachache walikuwa wakishawishi watu juu ya mambo madogo sana, awamu hii wamefeli. Reli inajengwa, waliobomolewa ni watu ambao walikuwa wanakaa katika maeneo inayotakiwa kupita reli kisheria.

Leo hii hawa hawa baada ya muda watakuja kuwaambia wananchi 2019/2020 kwamba wao ndio waliopiga kelele standard gauge imejengwa hao ni wadandiaji wa treni, na wanaidandia treni kwa mbele wala tusiwe na mashaka nao safari hawatafika wanakokwenda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo na mimi nilikuwa na michango michache sana.

Jambo la kwanza, naomba tutumie fursa, dada yetu Leah amesema ya maduhuli, Halmashauri zetu hizi zina minada mizuri kule katika Halmashauri, kwa mfano, Halmashauri yangu ya Kishapu, mimi ninaomba sana Mheshimiwa Waziri Jafo nikushauri ndugu yangu, tuna mpango mzuri sana Kishapu wa kutanua ile minada yetu na kuifanya minada ya kimataifa, tunakutana na kikwazo cha minada iliyoko sasa, iko chini ya Wizara ya Mifugo, tukienda kuomba minada ile tunaambiwa kuna madeni machache yanalipwa. Kishapu tuko tayari kulipia deni letu kama wanadaiwa ili tuachiwe ile minada na sisi tutanue own source zetu za ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikuombe sana Mheshimiwa Naibu Waziri na Mheshimiwa Waziri, hoja hii ni yenu TAMISEMI ongeeni na Wizara ya Mifungo mtupatie mnada wa Muhunze na minada mingine. Sisi watu sharp tuitanue ile miradi iwe sharp na iweze kuingizia mapato makubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ya Chama cha Mapinduzi imefanya kazi kubwa sana na kwa kweli katika dini yetu sisi waislamu tunasema Faa-mma biniimati rabbika fahaddith na tuzisimulie neema za Mungu zilizoko juu ya ardhi. Neema iliyoko Tanzania kwa Serikali ya John Pombe Joseph Magufuli sio ndogo. Serikali hii imeleta miradi ya ndege zetu wenyewe tunajenga reli ya kisasa, tunapanua bandari, tunajenga barabara, tumeleta Makao Makuu Dodoma ili Watanzania wote wanapohitaji huduma za Serikali waweze ku-connect… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)