Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, naomba niongelee mwenendo wa maduhuli katika Halmashauri zetu. Ni dhahiri kwamba Halmashauri za Wilaya, ufanisi katika ukusanyaji wa mapato umekuwa wa kusuasua, Halmashauri katika mikakati yake ya kukusanya mapato imekuwa ikionesha lakini changamoto wanayoipata ni kutokuwa na sheria ndogo na sababu ya kutokuwa na sheria ndogo wamekuwa wakisema kwamba sheria zinacheleweshwa kusainiwa TAMISEMI. Hivyo nitoe wito TAMISEMI iwaishe kusaini sheria ndogo ili ufanisi wa mapato uongezeke.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilifuta baadhi vyanzo vya mapato ambazo vilikuwa kero katika bajeti ya mwaka 2017/2018 na ninaamini Halmashauri pamoja na Serikali Kuu zilifanya mapitio katika bajeti zao. Lakini cha kusikitisha Halmashauri zinaendelea kutoza mapato kwa vyanzo vilivyofutwa. Kwa mfano Halmashauri hiyo hiyo ina ushuru wa pamba imepunguza asilimia mbili, kwa hiyo inatoza asilimia tatu, lakini Halmashauri hiyo hiyo inaendelea kutoza chanzo kilichofutwa kwa mfano kusafirisha mifugo ndani ya Wilaya. Ukimuuliza mkurugenzi kwa nini anafanya double standard anasema hana mwongozo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini Mkurugenzi asitumie kigezo alichotumia kuteremsha ushuru wa pamba akatumia hicho hicho kigezo kutoza ushuru wa kusafirisha mifugo. Hapa tunawaonea wananchi wetu na tunawaweka katika matabaka. Kwa hiyo ninaomba Wizara husika ilete miongozo ili halmashauri ziweze kurekebisha sheria ndogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.