Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi hii yakuchangia kwenye hoja iliyoko mezani. Mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Utawala Bora na Serikali za Mitaa na naunga mkono hoja ambayo imewasiliswa hapo mezani na ninawapongeza wote ambao wamewasilisha hoja zao hapa mezani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nitajikita katika maeneo mawili. Katika lile zoezi la vyeti fake kuna watumishi kama 11,696 ambao walitolewa kazini na kati ya hao 3,301 wametoka Serikali za Mitaa. Kwa sababu hiyo sasa upungufu wa watumishi katika Serikali za Mitaa umeruka kuanzia asilimia 51 mpaka asilimia 54 ambayo ni karibu watumishi 57,700.

Sasa ningependa kujua Mheshimiwa Waziri wa Utumishi kuna mkakati gani wa kuhakikisha kwamba serikali za mitaa zinapata watumishi ili kupunguza matatizo katika yale maeneo ya social services? Hilo la kwanza,

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili, pia tungependa kujua nini hatima ya hawa watu ambao wamekutwa na vyeti fake? Najua kweli wamevunja sheria lakini wengine wamekutwa na haya maswahibu karibu wanastaafu na wameitumikia nchi hii kwa muda wote. Je, nini hatma yao? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili linahusu wale waliotolewa waliomaliza darasa la saba ambao alishindwa kuendelea mpaka form four, kwa utaratibu wa kawaida hawa watakuwa wamestaafishwa. Tungependa kujua, je, serikali ina mpango wa kuwalipa mafao yao kwa sababu wamestaafishwa? Naomba Mheshimiwa Waziri akija atueleze nini hatma ya watumishi hawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni la mabasi ya mwendo kasi. Serikali imeanzisha huu mradi ambao ni mzuri ilianza vizuri, na lakini sasa hivi hali si nzuri. Si nzuri kwa sababu mabasi yanakuwa machache wakati wa peak hours watu wanasukumana kugombe ndani ya basi; na lengo la huu mradi lilikuwa ni kufanya usafiri uwe rahisi maana yake kama tunafuata kweli rappid transport kama ilivyo katik anchi za wenzentu basi hilo haliwezi kukaa muda mpaka lijae kama daladala. Inatakiwa watu wasafiri wakiingia hao hao walioingia wanaondoka linakuja basi lingine, linakuja basi lingine. Lakini mpaka sasa hivi huduma zimedorora.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tungependa kujua Serikali ina mkakati gani katika kuboresha huo usafiri wa mabasi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, inahusu karakana ya haya mabasi ya mwendo kasi. Inashangaza kwamba Serikali imewavunjia wananchi waliokuwa kwenye Mto Msimbazi, nyumba zao zikavunjwa. Hata hivyo ajabu ni Serikali yenyewe inajenga karakana ya mwendo kasi katika Mto Msimbazi. Mafuriko yalipokuja mwaka 2017/2018 lile eneo lilifurika, zile ofisi zilifurika maji mabasi yalikuwa kule ndani, vyombo vikaharibika mabasi yakaharibika na kuisabisha Serikali hasara kubwa. Je, Serikali itakuwa na mpango gani sasa kuona kwamba hatua zinachukulia ili kuepusha tena majanga mengine mvua nyingi zitakaponyesha katika lile eneo la Bonde la Msimbazi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ten percent katika Halmashauri zetu. Halmashauri nyingine zimekuwa zinafanya vizuri. Lakini Halmashauri zingine zilikuwa hazitengi ile asilimia 10 inayotakwa kwa ajili ya wanawakena vijana maeneo mengine wamefanya vizuri, maeneo mengine hawajafanya vizuri. Tunapendekeza, kama ilivyosemwa katika taarifa yetu, kwamba ingekuja sheria ambayo italazimisha Halmashauri ziweze kutenga hiyo asilimia 10 ya vijana na wanawake ili wananchi waweze kujiweka katika makundi na kuchangia katika uchangia katika maendeleo yao.

T A A R I F A . . .

Mheshimiwa Mwenyekiti, nne na nne jumlisha na mbili ni kumi, ahsante.