Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Jaku Hashim Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. JAKU HASHIM AYOUB: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nisikupotezee muda, mimi nitahitaji maelezo maana nikichangia itachukua muda mrefu, nitahitaji maelezo kwenye mambo kama manne Mheshimiwa Waziri. Nikupongeze tu juzi nilikuona katika sherehe za Siku ya Sheria Duniani na ulihimiza sana Mheshimiwa Waziri, mahabusu sheria ya kesi zao zile haraka, hebu tueleze kuna tatizo gani Arusha kule watu wana miaka sita mpaka leo wanachunguzwa nini? Kesi mpaka leo au kunatakiwa ushahidi wa Kinyamwezi mpaka ukamilike? Watu wanateseka, wana familia zao, wana watoto, wengine wanataka kuthubutu kuachwa, hebu tueleze tatizo ni nini? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kumejitokeza tatizo hivi sasa Zanzibar watu kuchukuliwa wakaja kushitakiwa huku Bara, je, Zanzibar hawana Mahakama? Hawana wanasheria? Tatizo gani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, na sheria inavyosema unapokamatwa ndipo unapohukumiwa. Leo sijaona mimi mtu kakamatwa Pakistan akaletwa Tanzania, kakamatwa Mascut akaletwa huku, hebu tueleze utaratibu gani wa sheria huu, ukoje? Mimi si mtaalamu wa sheria, lakini haya mambo yanajitokeza sasa hivi na yanazidi kuendelea, keshokutwa usije ukanichukua mimi ukanileta huku. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini na lingine nikuombe, hebu katika hiyo orodha ya mambo ya Muungano, na hii Mheshimiwa Chenge ulikitunga wewe kitabu hiki ukiwa Mwanasheria mwaka 2005. Kuna orodha hii ya mafuta na gesi, mali pamoja na mafuta yasiyochujwa na matokeo ya mafuta aina ya petroli na aina nyingine ya mafuta, limo humu na sheria hii ilivyoelezwa, angalia Ibara ya 64 Mwanasheria Mkuu na Waziri wa Katiba na Sheria; “Endapo sheria yoyote iliyotungwa na Baraza la Wawakilishi inahusu jambo lolote katika Tanzania Zanzibar ambalo liko chini ya mamlaka ya Bunge, sheria hiyo itakuwa ni batili na itatanguka na pia endapo sheria yoyote itakayotungwa na Bunge inahusu jambo lolote ambalo liko chini ya mamlaka ya Baraza la Wawakilishi, sheria hiyo itakuwa ni batili na itatanguka.”

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi ni vichekesho, kwa hiyo bado tuna mtihani wa mafuta Zanzibar. Pamoja na jitihada zilizochukuliwa, niwapongeze Marais wote wawili, lakini bado, na ulijibu hapa, ulimjibu Mheshimiwa Juma Ngwali kuwa bado mafuta ni tatizo. Hebu lipate kuliondoa ili Muungano ulete sura nzuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na lingine, mara nyingi waislamu wamekuwa wakiahidiwa Mahakama ya Kadhi humu ndani hebu tueleze imefikia wapi? Hata katika Katiba Iliyopendekezwa na wewe ulikuwa ni Mjumbe katika Tume ya Warioba, hebu tuelezeni juu ya Mahakama ya Kadhi nayo ina mambo matatu, ndoa, mirathi na talaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, watu wamekuwa wakilalamikia suala hili, na hili Bunge hili ukifuata Hansard limezungumza ndani wakati wa Mheshimiwa Mizengo Pinda kuwa, utaratibu fulani utaletwa, lakini mpaka leo? Imekuwa kama mtoto wa kuku anayetaka kunyonya, kesho, keshokutwa mpaka anakuwa kuku, maziwa hayaoni. Hebu tuelezeni lini utaratibu huu utaletwa wa Mahakama ya Kadhi? (Kicheko)

Mheshimiwa Waziri ulikuwa Mjumbe katika Tume ya Warioba na waislamu wengi walizungumzia suala hili. Kuna mambo ya ndoa, talaka na kuna mambo ya mirathi, hebu tuendelee na utaratibu wa kulieleza suala hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nisikupotezee muda. Naomba nafasi hii umpe mtu mwingine achangie dakika zilizobaki.