Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Jumanne Kibera Kishimba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kahama Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE JUMANNE K. KISHIMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana nitaenda moja kwa moja kwenye Serikali za Mitaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Halmashauri yangu ilipata hati safi kwenye ukaguzi wa CAG vile vile kwenye mwenge tulikuwa washindi wa pili au wa tatu. Lakini kitu cha kushangaza ripoti ya Mkaguzi wa Ndani wa Halmashauri inaonyesha tuna upotevu wa zaidi ya milioni 200 na zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa najaribu kujiuliza hapa kwamba inawezekanaje tuna hati safi kwenye mwenge tumekuwa wa pili au wa tatu lakini mkaguzi wa ndani kwenye ripoti ambayo ninayo hapa anaonyesha tuna upotevu wa zaidi ya milioni 200 na zaidi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama haitoshi Mkurugenzi wetu wa Halmashauri ameendelea kuwaburuza Madiwani kwa kutumia ubabe kiasi ambacho ameweza kuidhinisha ujenzi wa jengo la mamalishe lenye thamani ya shilingi milioni 200. Jengo hili kwa gharama ya shilingi milioni 200 lina mapato ya shilingi 120,000 kwa mwezi. Kwa hiyo faida ya kurudisha jengo hili litachukua zaidi ya miaka 200. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa namwomba waziri atakapokuwa anafanya majumuisho ajaribu kuangalia kama Serikali inakopa pesa, pesa hizo hizo milioni 200 ilizokopa kwenye mabenki ya ndani kwa riba ya asilimia kumi yenyewe italipa milioni 20. Ni vipi imeipatia Halmashauri ikajenga jengo la milioni mia mbili itapata return baada ya miaka 200 na itapata shilingi milioni 1.4 kwa mwaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiacha ubadhirifu huo unaoendelea kwa hao watu wanaitwa wateule wa Rais, Mkurugenzi huyu mpaka leo amekataa kutoa statement za benki, Mkuu wa Wilaya hawezi kumhoji, TAKUKURU hawezi kumhoji, Mkuu wa Mkoa hawezi hata sisi kamati ya fedha amekataa na kichekesho hapa ninapoongea anaendelea kupiga machinga wote wa Kahama. Namshukuru Mkuu wa Polisi amekataa kutoa polisi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa mji wetu wa Kahama watu walioajiriwa hawafiki watu 200, na mji ule una watu zaidi ya laki tano, ni kweli watu hawa watafanya shughuli gani? Hata hivyo Mheshimiwa Rais alisharuhusu machinga na watu wa kawaida waendelee na shughuli zao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri Jafo wakati anafanya majumuisho ajaribu kutueleza tutafanya nini au tushitaki wapi sisi? Maana hatuna sehemu yoyote ambayo tunaweza kulalamikia. (Makofi)

T A A R I F A . . .

MHE. JUMANNE K. KISHIMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naipokea hoja yako vizuri nafikiri Mheshimiwa Jafo uko hapo. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukweli sisi ni Wabunge, lakini mtu ambaye anasema yeye ni mteule anapojaribu kuwa- disturb watu waliokupigia kura anatupa sisi wakati mgumu sana. Tunajaribu kila namna kutafuta pesa kutoka kila kona, ili tusaidie watu wetu, lakini mtu anafika anakataa au ana- misuse hizi pesa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi tuna ongezeko la wanafunzi kwenye kidato cha kwanza zaidi ya asilimia 200; kwenye darasa la kwanza tuna ongezeko la asilimia 200 pia, tuna upungufu wa matundu 2,000 ya choo, lakini Mkurugenzi huyu amechukua pesa hizo milioni 200 amepeleka kwenye jengo la mama lishe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na hivi ninavyoongea Mheshimiwa Jafo ulipokuwa Naibu Waziri ulitoa agizo kwamba, wakati Wabunge wako Bungeni Kamati za Fedha zisikae, lakini yeye anaitisha Kamati ya Fedha kesho, ameongeza shilingi milioni 40 tena kupeleka kwenye jengo hili kwa ajili ya kuweka vigae. Kwa hiyo, naomba sana mtusaidie maeneo haya ni maeneo ambayo yanatupa matatizo makubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kumalizia tu naomba Mheshimiwa Jafo na Mheshimiwa Kakunda kwa kuwa mlifika Kahama mtufikirie sana suala letu la Manispaa. Ni kweli mji wetu umekua, mmeuona kwa macho na matatizo tuliyonayo. Mkitusaidia Manispaa itatusaidia vile vile kwa tatizo la barabara ambalo kwa sasa ni tatizo letu kubwa.