Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Niende moja kwa moja kwenye hoja kwanza niwapongeze wawasilishaji wetu Wenyeviti wa Kamati zote tatu kwa maana ya sheria ndogo, huduma za jamii pamoja na katiba na sheria. Niseme kidogo kuhusu kwa nini tunatunga sheria? Tunatunga sheria kwa ajili ya kuleta utengamano katika jamii pia kulinda haki za watu wote na hasa wanyonge. Hii ni tafsiri tu ya mtu ambaye yuko mtaani sio msomi lakini kwa ujumla hiyo ndio tafsiri ya sheria. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nampongeza Mheshimiwa Dkt. Magufuli amekuwa makini sana katika kuzingatia utawala wa sheria, ni mwepesi sana. Tumeona hapa kila tunapopitisha sheria mara moja anazisaini kwa sababu anataka kwenda kuzifanyia kazi ili kuendeleza huu utawala wa sheria. Pia amekuwa mkali sana Mheshimiwa Rais hasa kwenye sheria hizi ndogo, ukichelewa kutunga kanuni ninyi watu ambao mmepewa mamlaka ya kutunga kanuni hizi Mheshimiwa Rais amekuwa mkali sana. Mmeshuhudia hivi karibuni sheria nyingi ambazo zimetungwa ambazo hazijawekewa kanuni Mheshimiwa Rais amekuwa mkali sana.

Mheshimiwa Mweyekiti, kwa utangulizi huo labda niseme tu mafupi kuhusu sheria ndogo. Nizungumzie tu umuhimu wa sheria ndogo. Sheria ngogo ni muhimu sana, ni sawasawa na sheria mama zile ambazo zinatungwa. Huwezi ku-apply sheria mama kama hujatunga kanuni, haiwezekani, itakuwa dormant ndio maana Mheshimiwa Rais amekuwa mkali kwamba tumetunga sheria hii mbona hamjaniwekea kanuni ili niweze kutekeleza sheria hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia katika uchambuzi wa mimi ni mmoja wa wajumbe wa Kamati hii ya Sheria Ndogo, katika uchambuzi wetu tumegundua mambo mengi sana ambayo tumesomewa hapa. Tathmini yangu karibu asilimia 50 ya sheria ndogo ambazo zimekuwa zikipita kwenye kamati yetu kwa kweli zina makosa. Sample hii naipeleka kwa nchi nzima kwa ninyi mliokasimiwa mamlaka haya ya kutunga kanuni kwa mujibu wa Ibara ya 97 naomba sana muwe makini kwa sababu mnapokuwa mnafanya makosa kwenye utungaji wa kanuni hizi zinakwenda kujeruhi wananchi, zinakwenda kuumiza watu. Kwa mfano tumeona ushuru wa mazao, kwa mfano mzuri hapa mwezi Julai wakati Waziri wa Fedha anasoma hotuba yake ya bajeti alisema mazao ya biashara ushuru utozwe asilimia tatu na ya chakula asilimia mbili lakini kuna Halmashauri bado zinatoza mpaka asilimia tano. Hii ni mbaya sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeletewa hapa tumejaribu kuangalia tumeshauri ikiwezekana wakati mwingine wapewe adhabu hawa wanaosimamia vitengo hivi vinavyotunga hizi kanuni zinaumiza wananchi wazingatie haya maoni. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizitake tu mamlaka kwa ujumla zote Wizara zote, agencies zote na mamlaka zote ambao wamekasimiwa mamlaka haya ya kutunga hizi kanuni wawe makini sana. Tumeona mfano wa hiyo Sheria ya Nzega ile ya Hifadhi ya Mazingira ni ya ajabu sana, unazungumzia Ziwa Tanganyika wewe upo Nzega. Mita 60 kwamba m-preserve mita 60 msilime ndani ya mita 60 kutoka ukingo wa ziwa, hii ni mbaya sana.

Mimi ningekuwa Mheshimiwa Waziri ningekuwa nimeshampa adhabu huyo ambaye alikuwa amesimamia kutunga hii sheria ndogo, hii ni mbaya sana inaonyesha watu wanaumia sana hasa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia hii copy and paste watu hawasomi, hizi sheria zinapita maeneo mengi sana lakini mpaka waziri analetewa kusaini kitu kama hichi ni ajabu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hayo machache naunga mkono hoja zote tatu nashukuru sana.