Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Amina Saleh Athuman Mollel

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo na Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, nipo na nakushukuru sana kwa kunipa nafasi na moja kwa moja kwa sababu dakika ni chache niende kwenye kile nilichoandaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ibara ya 13 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasema kwamba watu wote wana haki sawa mbele ya sheria na Mtanzania yeyote hapaswi kuchukuliwa kama mhalifu mbele ya sheria mpaka atakapotiwa hatiani na mamlaka husika ambayo ni mahakama. Vilevile Ibara ya 107 inasema kwamba inatambua mamlaka pekee yenye haki na wajibu wa utoaji haki ni mahakama ya Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimenukuu vipengele hivi na hasa nikienda katika Wizara ya Katiba na Sheria ambayo ndio inayohusika na marekebisho ya sheria mbalimbali na mimi nitazungumzia Sheria ya Usalama barabarani (Road Traffic Act) ambayo ni ya zamani sana ya mwaka 1968 na moja kwa moja naomba nizungumzie kero iliyopo ambayo imekuwa sasa hivi ni kero kubwa sana inayosababishwa na askari wa usalama barabarani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama tulivyosema Ibara hiyo ya 13 na 107 lakini niulize tu na wakati Mwenyekiti wa Kamati husika atakapokuja hapa pengine atusaidie sisi ambao kwa namna moja au nyingine mambo ya sheria siyo sana. Ni mamlaka gani hasa ambayo inamruhusu askari wa usalama barabarani pamoja na kwamba taratibu hizo zipo lakini nataka kufahamu ni sheria gani ambayo inamruhusu anaposimamisha tu gari moja kwa moja kudai leseni? Vilevile hapo hapo kuanza kuandika notification kutokana na vitu mbalimbali ambavyo ameviona?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano hivi sasa na hata ukiangalia katika Jiji la Dodoma hebu watusaidie ni sheria gani ambayo inamtaka dereva asimame wakati wowote anapofika kwenye zebra crossing. Kwa sababu ni busara tu kwamba anapofika kwenye zebra crossing kama kweli kuna watu ambao wanavuka pale barabara sawa lakini wakati mwingine hakuna hata mtu anayevuka barabara na anapopita katika eneo hilo moja kwa moja tayari askari anamsimamisha na kumwandikia faini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sio hilo tu askari anapofika kitu cha kwanza anaomba leseni. Sasa mtusaidie sisi ambao hatujui sheria na Watanzania wengine wote kwamba ni sheria gani ambazo zinamfanya askari wa usalama barabarani kujichukulia sheria yeye na kuandika faini na wakati mwingine mtu anaandikiwa makosa mpaka manne, matano na hasa anapokuona kwamba kwa namna moja au nyingine wewe kidogo unauelewa wa sheria anachukulia kama ni kisasi na ndipo hapo anapoandika makosa mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano mtu anakwambia washa taa kwa mchana hivi jamani tuna haja kweli ya kuwalazimisha watu kuwasha taa na kama hiyo taa labda ina matatizo tayari moja kwa moja hapo hapo anakwandikia notification. Tumeona hapa kama nilivyosema hizo Ibara ya 13 na 107 vyote hivyo angalau basi mamlaka zinazohusika ndizo ambazo zinapaswa kuhakikisha kwamba makosa hayo yanafanyiwa kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwa sababu sheria hizi ni za muda mrefu sana tunaomba mabadiliko ya sheria yaletwe na kama Serikali bado inaona kwamba kuna wakati mgumu au kuna kigugumizi tuombe basi mwenyekiti wa Kamati husika, kwa sababu na wao pia kwa mujibu wa sheria zinamruhusu kufanya hivyo waahirishe na kuleta kwamba vile ambavyo vinahitaji kufanyiwa marekebisho iliā€¦

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. AMINA S. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.