Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Luhaga Joelson Mpina

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisesa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana, kwa nafasi ambayo umenipatia, na nianze kwa kuwapongeza sana Kamati yangu hii Kamati ya Kilimo, Maji na Mifugo ambayo inaendeshwa na akina mama, nawapongeza sana kwa uendeshaji wa Kamati hiyo vizuri sana Mheshimiwa Mwenyekiti wetu Dkt. Mary Nagu pamoja na Mheshimiwa Dkt. Ishengoma ambaye ni Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wa Kamati kwa weledi wao mkubwa sana katika kutusimamia na kutuongoza kutekeleza majukumu yetu. (Makofi)

Mheshimiwa mwenyekiti, najua zipo changamoto nyingi sana ambazo zimezungumzwa na Waheshimiwa Wabunge na kwa dakika 10 haitatosha sana kuzijibu, lakini nijaribu kusema kwa kifupi kwamba Kamati hii yangu ambayo imewasilisha taarifa hapa chini ya Mwenyekiti wake, imezungumizia juu ya kushughulikia changamoto ambayo zinahusu viwanda vyetu vya maziwa hapa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunafahamu changamoto ya maziwa hapa nchini tunafahamu tatizo la uingizaji maziwa ambao leo imefikia zaidi ya kilogramu milioni 88 ya uingizaji wa maziwa kutoka nje ya nchi na kusababisha ushindani usio sawa katika Taifa. Tunafanya tathmini na tutapata majawabu. Lakini vilevile wamezungumza suala la Ranchi za Taifa (NARCO) kwamba tufanye tathmini tujue uwekezaji uliopo, tujue changamoto zilizopo ili tuweze kuja na mapendekezo sahihi ya namna bora ya kuwekeza katika eneo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeunda Kamati hiyo tayari chini ya maagizo hayo hayo ya Kamati hii ilivyotuelekeza tukaunde Kamati na kamati hii imeshamaliza kufanya tathmini, kesho napokea ripoti ikiongozwa na Mheshimiwa Archad Mutalemwa DG Mstaafu wa DAWASA na kesho napokea taarifa hiyo na tutakapoipokea hiyo taarifa tutaenda mbele ya Kamati yetu kushauriana nayo au kama kuna input zingine ili tuweze kwenda mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uvuvi haramu, nishukuru sana Kamati yetu imetupa msukumo mkubwa katika ukurasa wa 32 ya kwamba tuongeze bidii katika kupambana na uvuvi haramu, lakini tuongeze bidii katika kuhakikisha kwamba wale wanaotorosha samaki wetu mazao ya samaki, tunawadhibiti ilivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niihakikishe Kamati kwamba na Wizara yangu, tutahikisha hili tunalisimamia kwa nguvu zote, hizi ni rasilimali za Taifa, na rasilimali hizi haziwezi kuwa shared kwa ukanda. Rasilimali hizi zinakuwa shared kwa nchi nzima kwa hiyo kama Wizara, inayosimamia sheria ambayo zimepitishwa na Bunge hili, tutahakikisha kwamba hakuna kabisa uvuvi haramu katika nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile tutahakikisha hakuna mfanyabiashara atakayejihusisha na kuuza wala kusambaza zana haramu, hakuna kiwanda kitakachochakata samaki wasioruhusiwa, hakuna mtu yeyote atakayevua kwa kutumia nyavu haramu, lazima mali zetu tuzilinde kwa nguvu zote, na bila kumumunya maneno labda nitoe takwimu zilizopo kwa sasa hivi, tuko wapi katika rasilimali hizi za uvuvi, ukizungumzia Ziwa Victoria…

T A A R I F A . . .

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi natoa majibu hapa kwa maelekezo yake yeye au natoa majibu kwa mpangilio ambao ulioko hapa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ndio naanza kujibu tu sijafika hata mbali, anisubiri asikilize vizuri ninavyozungumza hili ni Bunge, mimi ni Mbunge na yeye mwenzangu huyu ni Mbunge, anisikilize vizuri. Sasa sijamaliza hata kuzungumza sijamaliza hata sentesi.

Mhesimiwa Mwenyekiti, sasa naomba kusema kwamba takwimu kwa sasa hivi katika Ziwa Victoria, linasema hivi, samaki ambao wanaruhusiwa kuvuliwa, sangara, ambao ni sentimita 50 mpaka sentimita 85 wamebakia asilimia tatu tu, kwa hiyo hata uvuvi huo tunaouzungumza hauwezi kuwepo kama uvuvi haramu huu tutauruhusu. Samaki wazazi katika Ziwa Victoria wamebaki asilimia 0.4 huna wazazi, huna ziwa, huwezi kuvua samaki ambao leo sasa ambao ni wachanga na ndio wanaovuliwa, wachanga wasioruhusiwa, chini ya sentimita 50, ni asilimia 96.6.

Kwa hiyo, kwa mantiki hiyo hatuna samaki wanaofaa kuvuliwa katika Ziwa Victoria, Kamati imezungumza juu ya viwanda kufungwa tulikuwa na viwanda 13 hapa viwanda 13 vilikuwa na uwezo wa kuzalisha tani 1,065 leo tumebakiza viwanda nane na viwanda nane hivyo vina uwezo wa kuzalisha tani 171 tu. Sababu ya kukosekana kwa rasilimali hizi za uvuvi, samaki hawapo wamekwisha kutoweka kwa sababu ya uvuvi haramu, watu wanavua mpaka mayai, watu wanavua mpaka wachanga wale, utapata wapi samaki? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ajira zilikuwa 4000 na kitu leo ni 2000 tu katika ziwa letu hilo la Victoria, lakini nataka niseme hii operation ambayo inayoendelea na kama Waziri niliyeapishwa kusimamia rasilimali hizi kwanza niweke kabisa wazi msimamo wa Serikali kuwa wananchi wanaojishughulisha na wafanyabiashara wanaojishughulisha na uvuvi haramu waache, kwa sababu wakiendelea kufanya hivyo, rasilimali hizi zitatoweka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mpina hapa ni mlinzi tu, kibarua sitaenda kuvua Ziwa Victoria wataenda kuvua wananchi wa Geita, wataenda kuvua wananchi wa Chato, wataenda kuvua wananchi wa Mara, wataenda kuvua wananchi wa Mwanza, mimi sitabeba nyavu, nazuia wale samaki na Wizara yangu kazi yetu ni kuhakikisha rasilimali zile zinakuwepo wananchi wetu wafanye biashara vizuri, wavue vizuri, wale samaki wazuri, ndio kazi ya Serikali. (Makofi)

T A A R I F A . . .

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, utunze muda tu muda wangu ili usiingie ndani ya miongozo ambayo inaulizwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa katika operation hii, niliyoiunda ya operation katika Ziwa Victoria, operation sangara mwaka 2008, operation hii ina wataalam hafanyi maamuzi mtu mmoja, timu hii ina wavuvi, ina NEMC, ina TISS toka Ofisi ya Rais, ina TAMISEMI na ina Polisi.

Kwa hiyo, watu hawa wanafanya assessment mambo ya vipimo vya ngazi mbili, ngazi tatu hayo ni kwa mujibu wa wataalam wetu, wataalam wetu wapo wanaofanya maamuzi na kutushauri kama Serikali, sisi tunasimamia maamuzi hayo. Katika operation hii tuliyoyaona yanatisha, ziko gari za Waheshimiwa Wabunge tumezikamata na samaki haramu, wapo Waheshimiwa Wenyeviti wa Halmashauri, wapo wenyeviti wa vijiji tumefukuza watu tumesimamisha kazi watendaji wa Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hapa katika kufanya opetation hiyo, tulipokagua viwanda vyote, hakuna kiwanda hata kimoja tulichokikuta kinachakata samaki ambao wanaruhusiwa, vyote vilikuwa vinachakata samaki ambao wasioruhusiwa.
Tumekamata viwanda, tumekamata viwanda vya nyavu, viwanda vya nyavu ....

T A A R I F A . . .

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa ya awamu ya kwanza ya operation sangara mwaka 2018 inayoendelea iko karibuni mbioni hatua ya kwanza kumalizika na mimi mbele ya Kamati yangu, nilishaiahidi kwamba baada ya taarifa hii kutoka nita-share na Kamati na niki-share na Kamati itaaingia kwenye Bunge lako, hilo wala halina tatizo. Ninachotaka niseme sasa ni haya yafuatayo; katika operation tuliyoifanya…

T A A R I F A . . .

WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, labda niruidie kusema katika operation hii tumesimamisha watendaji wa Serikali waliokuwa wanajihusisha na uvuvi haramu, tumekamata baadhi ya magari ya Waheshimiwa Wabunge ambao wako humu humu Bungeni, tumekamata baadhi ya Wenyeviti wa Halmashauri, tumekamata na hata kuwaweka ndani baadhi ya Madiwani, na nasema hivyo sasa kwa mantiki hiyo, kama nilivyosema kwamba tunakamilisha taarifa, operation hii inafanyika katika mikoa mitano. (Makofi)

T A A R I F A . . .

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekamata zaidi ya kilo 133,000 zikitoroshwa kwenda nje ya nchi, za samaki aina ya kayabo na dagaa, 133,000 zikitoroshwa kwenda Rwanda, zikitoroshwa kwenda Burundi, zikitorosha kwenda Kongo na Sirari, zaidi ya tani 133,000. Tumekamata samaki wachanga zaidi ya kilo 73,000 rasilimali hizi zote zinachezewa kwa kiwango hicho. Tumekamata mpaka wageni walikuwa wanaingia mpaka kwenye visiwa vyetu wanashiriki uvuvi, wanunua samaki mpaka kwenye visiwa ambayo ni kinyume cha sheria wageni kutoka Rwanda, wageni kutoka kutoka kutoka Kenya, wageni kutoka kutoka Burudi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tumekamata viwanda, vilikuwepo hapa viwanda vya mabondo 22 vinafanya biashara ya mabondo lakini vilivyokuwa na leseni halali vilikuwa viwili tu. Kwa hiyo, tukisema tunapambana na uvuvi haramu, tunapambana nao kweli kweli na hii operation yangu hii haina mwisho hadi uvuvi haramu utakapomalizika hapa nchini mwetu na kwamba uvuvi wa wa bahari kuu na kwenyewe tumeshapata ya kufanya doria katika uvuvi wa bahari kuu walikuwa wamezoea wanavua wanaondoka Taifa letu linaachwa halina chochote. Tunashindwa kukusanya chochote na ndio maana mara ya kwanza tu nimeenda kukamata meli ile ambayo tumeikamata na tumepiga faini shilingi milioni 770.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitegemea Bunge hili litapongeza jitihada hizi kubwa za Wizara ambazo zinalinda rasimiali hizi, leo hii mkakati wa kulinda uvuvi wa bahari kuu tutazikagua meli zikiwa zinaendelea kuvua huko huko, hakuna mtu atakayeondoka kwenye maji ya Tanzania akiwa amebeba rasilimali ya Watanzania na tutaongeza meli zingine mbili za doria, tunahikisha kwamba uvuvi wa baharini kuu pamoja na bahari nzima, coastal nzima yetu inalindwa kwa nguvu zote kuhakikisha kwamba rasilimali hizi nchini mwetu, Serikali hii ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zote rasilimali hizi zinanufaisha Watanzania, hatarusiwa mtu yeyote. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyeki, niseme nasema kabisa hapa kama mtu atajishirikisha na uvuvi haramu hata mimi Mpina hata Mzee Mpina mwenyewe ninyi doria mkamateni kama anajishughulisha na uvuvi haramu wa Taifa hili. Hatuwezi kuongelea kwa maneno mapesi katika rasilimali za Taifa, sisi kama Serikali ni walinzi tu, makolokoloni, kolokoloni ukikuta mlango wa tajiri umevunjwa una shida kubwa, mimi ni kibarua wenu, kazi yangu ni kuhakikisha katika wizara mliyonipa rasilimali zinalindwa kwa nguvu zote na kazi hiyo na wizara yangu tutaifanya usiku na mchana. Lakini nasema kama kuna hoja ya msingi Wabunge wasituhumu kwa jumla, yawezekana kuna mtendaji akakosea katika kuchukua hatua unasema katika eneo fulani, katika kijiji fulani, kuna jambo hili na hili limefanyika Mpina - Waziri lishughulikie hata sasa hivi ukiniletea nitafanyia kazi na kuchukua hatua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, rasilimali hizi za Taifa zimetoroshwa kiasi cha kutosha na ninyi hapa Bunge hili muda wote limekuwa likilia makusanyo ambayo tunakusanya Halmashauri na Wizara kuhusu uvuvi ukijumlisha sisi sote ni takribani shilingi bilioni 20 ukiwaondoa wenzetu labda wa TRA. Kwa hiyo, makusanyo ni hafifu licha ya bahari kubwa tuliyonayo, licha ya maziwa tuliyonayo, licha mito tuliyonayo kwa hiyo ni wakati sasa wa Bunge hili kuisaidia hii Wizara, vijana hawa wanaofanya doria wanafanya kazi ya kujitolea sana, wangekuwa wepesi wasingeweza kufanya hatua kubwa hizi ambazo wanazozichukua sasa hivi.