Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono taarifa ya Kamati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niipongeze MVIWATA kwa kazi kubwa wanayoifanya kutoa ushauri, elimu kwa wakulima hapa nchini. Pamoja na hayo, niombe Halmashauri zetu kuunga mkono kazi wanayofanya kama vile kuunda vikundi vya umoja, kujenga masoko ya kuuzia mazao yao. Hivyo, nishauri Serikali kuunga mkono juhudi za MVIWATA kwa kutatua changamoto zilizopo hivi sasa kama ifuatavyo:-

(i) Kurejesha kwa wakati gawio la ushuru wa asilimia 35 wa kuendesha shughuli za masoko kwani Halmashauri nyingi hazirejeshi;

(ii) Kukarabati barabara za vijijini zinazokwenda kwenye masoko;

(iii) Kuzuia wakulima kuuza mazao yakiwa shambani;

(iv) Kuzuia mazao yanayozidi kilo 100 kama vile rumbesa;

(v) Kupunguza kodi ambazo ni utitiri kwenye vikundi vya SACCOS ambavyo vinaendesha masoko;

(vi) Kuweka ulinzi kwenye njia za panya wanazotorosha mazao bila kulipa ushuru.

(vii) Kupeleka mbolea kwa wakati;

(viii) Serikali itoe elimu kwa vikundi vya MVIWATA;
na

(ix) Kujenga viwanda vya kuchakata mazao.