Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kurejea kauli mbiu ya Mheshimiwa Rais wetu ya kuwatua ndoo ya maji kichwani wanawake, ambayo Wizara imejipanga kuifanyia kazi lakini itachukua muda mrefu kufikia vijijini ambako wananchi wengi wazalishaji wanakoishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashindwa kuelewa kwa nini Serikali inakuwa na kigugumizi cha kukubali ushauri wa Sh.100 kwa lita ya dizeli na petroli, kwa ajili ya Mfuko wa Maji Vijijini. Kwa sasa na kuelekeza nguvu zaidi ya utekelezaji wa ukamilifu wa miradi ya maji kwani hata vyanzo vya maji vipo vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba ushauri huu wa Sh.100 utekelezwe ili kuharakisha kauli mbiu ya Mheshimiwa Rais ya kuwatua ndoo wanawake. Ukimtatulia tatizo la maji mwanamke utakuwa umeitatulia jamii nzima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati za Maji zinasisitiza umuhimu wa uwakilishi wa mwanamke ndani ya Kamati hiyo. Tunashauri kuanzishwa na kamati za kutunza vyanzo vya maji vijijini zenye ushirikishi wa wanawake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuwepo na ufuatiliaji na uthamini wa vyanzo hivyo na kuviweka katika madaraja ya ushindani ambako kutahamasisha utunzaji wa vyanzo na kuwa endelevu. Tutaepukana na ukosefu wa maji na wananchi watapata maji safi na salama kwa gharama nafuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo ndilo tegemeo letu hapa nchini kwa ajili ya upatikanaji wa bidhaa ndani ya viwanda vyetu vya uzalishaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kuendelea kuchambua na kuona namna ya kuteremsha bei na kuboresha utaratibu rafiki zaidi kwa wakulima wetu katika upatikanaji wa pembejeo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kuona umuhimu wa kuongeza Maafisa Ugani wa kukidhi mahitaji na kuleta tija kwa wananchi wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kadri tunavyojipanga kuboresha kilimo na kuzalisha kwa ziada na kuingiza kwenye biashara na kukosa soko kutokana na nchi zinazotuzunguka nao kuanza kuzalisha hayo mazao ya kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, wataalam wa uwekezaji kuona utaratibu wa kukinzana na hali ya wakulima kuhangaika na mazao yao na kuona kilimo ni tatizo kwao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.