Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipongeza Kamati kwa kazi nzuri ya kufuatilia kazi kwa umakini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, michango. T.F.C ipelekwe Wizara ya Kilimo ili Wizara ya Kilimo iweze kuisimamia na kuifuatilia kwa karibu ili kuleta ufanisi wa kazi zake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Kilimo iweke utaratibu wa kukutana na wadau wote wa kilimo angalau mara mbili kwa mwaka ili kubaini matatizo na changamoto zinazokabili sekta ya kilimo. Pia, Benki ya Kilimo iongezewe mtaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu maji; kuwekwe utaratibu wa ufuatiliaji wa miradi ya maji kote nchini ili kuhakikisha vifaa na miundombinu ya maji vina ubora unaohitajika kwa mradi husika ili kubaini wakandarasi wasiofuata masharti na mikataba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tozo ya mafuta iongezwe iwe Sh.100 ili kuongeza mtaji katika Mfuko wa Maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu uvuvi; Serikali iharakishe ujenzi wa bandari ya uvuvi na ununuzi wa meli ya uvuvi.