Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Ignas Aloyce Malocha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. IGNAS A. MALOCHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, maliasili na utalii; naunga mkono taarifa zote mbili na mapendekezo yake yote. Migogoro ya hifadhi za akiba na wakulima itamalizika lini? Upo mgogoro mkubwa kati ya Hifadhi ya Uwanda na wananchi juu ya utata wa mipaka

Mheshimiwa Mwenyekiti, ipo ramani iliyokuwepo toka mwaka 1959 na ikafanyiwa marekebisho mwaka 1974. Cha ajabu ramani zote hizo zinapuuzwa na watumishi wa maliasili na kuingilia makazi ya wananchi. Naomba Wizara ifanye haraka kufanya makubaliano ya mipaka iliyowekwa Kisheria kwa kufuata ramani na siyo kukandamiza wananchi

Mheshimiwa Mwenyekiti, Maafisa wa Maliasili waliopo katika Hifadhi ya Akiba ya Uwanda hula rushwa na kuruhusu mifugo kukaa ndani ya hifadhi hiyo kwa kuwatoza wafugaji fedha kati ya milioni mbili na kuendelea bila kutoa risiti inakuwa ni fedha yao na haingii Serikalini. Majina ya Maafisa hao nilishayapeleka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, juzi Maafisa wa Maliasili wamefyeka mazao ya mwananchi mmoja aitwae Langi Lusangija Nonga, kisa kukataa kutoa rushwa. Naomba Serikali ifuatilie suala hilo

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanyama wanaodhuru; tarehe 9 Januari, 2018 Mamba amekamata mwananchi aitwae Didas Chendelwa katika Mto Momba. Maafisa wa Maliasili wamejulishwa juu ya jambo hili hawajachukua hatua yoyote na mamba hao wanazidi kutishia maisha ya wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi; soko la mahindi linawatesa wakulima wa mahindi. Serikali imewatelekeza wakulima wa mahindi hawana kwa kuuza mahindi yao. Leo hii Sumbawanga debe moja la mahindi ni Sh.3,500 hii siyo sawa kabisa. Serikali itueleze, je, hali hii itaendelea hadi lini?

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia kuna tatizo la pembejeo kuletwa kwa kuchelewa, uchache wa mbolea, bei kuwa kubwa ya pembejeo.