Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Joyce John Mukya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. JOYCE J. MUKYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuchangia katika hotuba ya utekelezaji wa Kamati kama nilivyoainisha hapo juu. Tatizo la maji linazidi kuwa kubwa siku zinavyokwenda. Hii siyo kwa baadhi ya maeneo ya nchi bali kwa nchi nzima. Mfano katika Wilaya ya Arusha Mjini mahali ninapoishi tatizo hili limekuwa sugu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la Njiro limekuwa na shida kubwa ya maji zinaweza zikapita hata wiki mbili au tatu bila kuona maji na wakati huo huo mvua zinakuwa zinanyesha. Nimeona kamati ilitembelea Mamlaka ya Maji AUWSA na kupewa taarifa kuhusiana na tatizo hili kama inavyoonekana katika ukurasa wa 45 -48.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naona niseme kuwa wahusika wa Mamlaka ya Maji Arusha Mjini hawakusema ukweli kwa Kamati kuwa tatizo kubwa la maji Arusha Mjini linasababishwa na tatizo la umeme. Hili alithibitisha Felix Mrema mwaka 2015 wakati wananchi ilipobidi waandamane ili kuweza kujua nini hasa tatizo la maji katika Jiji la Arusha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mahitaji ya maji katika Jiji la Arusha kwa siku ni lita milioni mia moja, (1000,000,000) lakini kutokana na mgao wa umeme uzalishaji umeshuka hadi kufikia lita milioni arobani na tano tu (45,000,000) kwa siku ambapo katika eneo la Moshono (Kata) uzalishaji umeshuka hadi kufikia galoni 100 kwa siku.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali ni mbaya sana katika nchi kwa ujumla kwa upatikanaji wa maji, ikizingatiwa Mkoa wa Arusha kuna Mlima Meru sijui maeneo ambayo ni makavu kabisa ikoje.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata nafasi ya kuchangia kwa maandishi.