Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeze taarifa ya Kamati, Mifugo na Maji. Napenda kuchangia kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo ningeshauri Serikali kusaidia wananchi kupata soko au masoko ya mazao yao.

Ningependa kuishauri Serikali juu ya uwahishaji wa pembejeo kwa ajili ya kuendana na wakati wa uhitaji. Tunaposema tutaondoa umaskini pamoja na kuwapa uhuru wa kuzalisha na kuuza kwa faida ili kurudisha gharama zilizotumika wakati wa kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali kutoa mikopo yenye riba nafuu kwa ajili ya kupata matrekta badala ya kilimo cha mkono kisicho na tija kwa jamii kinachosababisha vijana wengi kukata tamaa na kukimbilia mijini kutafuta fursa na wanapozikosa hugeuka wahalifu. Ningeshauri Serikali kuangali upya juu ya Mto Ruvu kutumika kikamilifu katika umwagiliaji ili kuwakwamua wananchi hao kuondokana na lindi la umaskini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali juu ya upigaji chapa mifugo kwani zoezi hili limeharibu soko la ngozi ambalo lilikuwa limeshamili sasa hivi limeporomoka ghafla badala ya ngozi za Tanzania kukosa ubora kutokana na chapa hizo. Nashauri Serikali kusaidia vijiji kuwa na majosho ya ng’ombe kama hapo awali miaka ya sabini ambapo uogeshaji ulifanyika kwenye majosho ya Serikali kwa kulipia ili kusaidia kupunguza vifo vya mifugo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali juu ya tatizo la maji ambalo ni lengo la Taifa kwani maeneo mengi ya Tanzania yana shida ya maji, hata yale ambayo vyanzo vyake viko bayana, ukiangalia utaona jinsi ambavyo wananchi wengi wanashirikiana na mifugo. Nashauri Serikali ifuatilie kwa karibu sana juu ya miradi ya maji ambayo inaendeshwa kwani inajengwa chini ya kiwango. Hivyo Serikali ifuatilie kwa karibu ili kuondoa pesa inayopotea. Nishauri kuwahisha fedha kwenye Halmashauri zetu ili ziweze kutumika kwa wakati.