Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Risala Said Kabongo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. RISALA S. KABONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa fursa ya kuchangia Wizara hii na kwa kunimheshimiwa mwenyekitipa pumzi ya kusimama hapa kwenye Bunge lako Tukufu leo. Nianze kwa kupongeza Kamati ya Ardhi Maliasili na Utalii kwa kupata fursa ya kufanya ziara za kutembelea baadhi ya vivutio vya utalii nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mambo muhimu ambayo kama mdau wa uhifadhi, ningependa kuyasisitiza ni Wizara hii kuwa na ubunifu. Kumekuwa na utalii wa aina moja miaka mingi, hivyo nashauri tuwe na aina nyingi za utalii ambazo zitafanya mtalii aache fedha zake, kuliko kutegemea fedha za lango kuu, wakati mgeni anaingia hifadhini. Mfano kivutio kilichopo Hifadhi ya Manyara ni mfano mzuri wa ubunifu. Nashauri maeneo mengine yafanye hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la vitalu vya uwindaji. Kumekuwa na sintofahamu kutokana na kauli mbalimbali za kuzuia na kuruhusu uendeshaji wa vitalu vya uwindaji. Kutokuwa na msimamo wa matamko katika Wizara hii kunaathiri shughuli nzima ya uwekezaji kwenye vitalu vya uwindaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hivi kwa sababu, biashara hii inauzwa au inafanyiwa masoko kabla ya mteja kutumia bidhaa. Hivyo, tunaweza kupoteza mapato mengi na kuwafanya wafanyabiashara ya utalii wa uwindaji kukata tamaa ya kuwekeza nchini. Mfano, leo tuna vitalu 61 havina wawekezaji, lazima tujiulize tumekosea wapi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la mipaka. Kumekuwa na migogoro ya uhifadhi na wananchi wanaozunguka hifadhi zetu. Kama hatutaweza kuweka suluhisho la mipaka yetu ya hifadhi, tunakwenda kuwaumiza wananchi wetu kwa kuendelea kuwatoza faini kubwa na adhabu mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kushauri kwamba Serikali kupitia Wizara ya Ardhi, Maliasili na Mifugo tuweze kukaa pamoja ili kuwa na mpango wa pamoja wa matumizi bora ya ardhi na kuweza kupunguza na kumaliza kabisa migogoro ya mipaka.