Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Grace Sindato Kiwelu

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. GRACE S. KIWELU: Naomba kuchangia machache katika taarifa ya Mjumbe wa Kamati hii. Naomba kuongeza machache katika katika maoni yetu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro ya ardhi katika maeneo ya Hifadhi ni tatizo kubwa sana katika vijiji vinavyozunguka hifadhi zetu. Hivyo ni jukumu la Serikali kuhakikisha migogoro hiyo inamalizika na kuleta uelewano kati ya wananchi na watumishi wa Hifadhi (Askari) zetu. Kama Serikali haitachukua hatua za haraka, migogoro hii itasababisha vurugu na hata kusababisha majeraha hata vifo kwa wananchi wetu. Hivyo, ni muhimu sana wananchi kushirikishwa na Wizara husika kwenye zoezi hili ili kufikia muafaka kwenye suala hili la mipaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wafugaji wamekuwa na malalamiko mengi kuwa Askari wa Wanyamapori wamekuwa wakiwanyanyasa sana kwa kuswaga ng’ombe zao kwa nguvu na kuziingiza kwenye hifadhi na kulazimishwa kutoa rushwa na wakishindwa kutoa rushwa hiyo mifugo yao hupigwa mnada. Ziko taarifa kuwa Askari hao kutumia ndugu zao kununua ng’ombe hao. Kama Kamati tumeliomba Bunge liunde Kamati Maalum kuchunguza tuhuma hizo ili ukweli ujulikane na sheria ichukue mkondo wake kwa wale watakaokutwa na hatia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu uvamizi wa mifugo katika hifadhi; katika ziara zetu tumeona jinsi vyanzo vya maji vikiharibiwa na mifugo na kukosekana kwa maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya mabwawa, malambo kwa ajili ya mifugo. Hivyo, tunaishauri Wizara husika kuweka malambo na mabwawa katika maeneo hayo ili kupungua au kumaliza kabisa suala hilo la uvamizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee kuweka msisitizo kwenye ushauri wa Kamati yetu kuhusu uundaji wa Kamati kujua ni kwa nini mapato ya Sekta hiyo ya Uwindaji yameshuka? Siyo Mheshimiwa Waziri kukimbilia kufuta leseni za vitalu ambazo tayari wawekezaji wameshalipia na kupata booking za wageni; leo ukiwaambia unawapunguzia muda wa leseni zao, itakuwa siyo sawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ziara zetu tumeona mapitio ya wanyama yamezibwa kwa shughuli za kibinadamu na hii imesababishwa na kutokuwepo kwa vibao vya kuonesha kuwa eneo hilo ni shoroba. Hivyo, tunashauri hifadhi zishirikiane na Halmashauri na Wizara zinazohusika kuweka mipaka na mabango kuonesha maeneo hayo ya shoroba ili kupunguza na kumaliza kabisa tatizo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hayo niliyochangia hapo juu na tukizingatia maoni yote ya Kamati, naamini migogoro inayoikabili sekta hii ya utalii itapungua na kwisha kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hayo machache, naomba kuwasilisha mchango wangu.