Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichangie hoja hii kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kumekuwa na migogoro ya ardhi katika maeneo mengi kwa sababu hayajapimwa na wanapotokea Wawekezaji huyachukua maeneo makubwa na wananchi wanabaki hawana ardhi. Pia Wawekezaji wengi wanachukua maeneo makubwa lakini hawajayaendeleza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano; Kanisa la KKKT katika Halmashauri ya Njombe Mjini ambao wamemilikishwa eneo la hekta 120 wanashindwa kuliendeleza. Naiomba Serikali ichukue maeneo ambayo hayajaendelezwa na yarudishwe kwa wananchi

Mheshimiwa Mwenyekiti, TANAPA, Shirika hili linawasumbua sana wananchi, mipaka iliyowekwa wameongeza na kuingia kwenye maeneo ya wananchi na kusababisha migongano kati ya wananchi na TANAPA. Niombe Serikali kuwaacha wananchi kwenye mipaka yao iliyowekwa zamani. Mfano, Wilaya ya Wanging’ombe, Kata ya Luduga kuna migogoro hiyo ya mipaka Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuishauri Serikali kuongeza bajeti ya Wizara ya Ardhi ili kuweza kupima ardhi na kupanga matumizi yanayofaa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.