Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napendekeza jitihada ya Serikali katika kutatua matatizo, migogoro na changamoto zinazokabili ndani ya Wizara ya Maliasili na Utalii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa wananchi kwa asilimia 80 wanatumia nishati ya kuni na mkaa na kuyumbisha uhifadhi wa misitu yetu hutupatia matatizo kadhaa kama vile ukosefu wa mvua, kutoweka kwa vyanzo vya maji pamoja na mito kukauka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, bado umeme na gesi kuwa na gharama kubwa na kutokuwepo ama nishati hizo hazijasambaa nchi nzima na zikiwa ndiyo nishati mbadala kwa wananchi wetu. Hivyo, ni vyema Serikali ikaharakisha kuleta Muswada wa Sheria ya Mbegu za Miti kuwa na bei rafiki na wezeshi kwa wananchi ili kuwawezesha wananchi kupanda miti ya muda mfupi kwa wingi na kuwezesha kuitumia kwa nishati na kurejesha misitu yetu kwa miti ya muda mrefu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wakala wa Mbegu za Miti wapewe Bajeti ya kutosheleza kuweza kufanya utafiti wa mbegu za miti na kubainisha upevu wa miti katika muda mfupi kwa kuharakisha kuondoa usumbufu utakaojitokeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, utafiti unaenda sambamba na kuwa na maabara bora zenye vifaa vya kisasa viendavyo na wakati uliopo na kuharakisha matokeo ya ubunifu wa wataalam wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa bado upatikanaji wa nishati mbadala kwa wananchi, basi Serikali ni vema ikawa na udhibiti kwa watumishi wanaotoa usumbufu, kujenga kero na chuki kwa Serikali na wananchi wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara/Serikali inajitahidi kushughulikia migogoro ya ardhi na hifadhi zetu kwa ujumla wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na kujipanga kwa kuboresha majiji katika muonekano wake ni sawa, ila nashauri Serikali kwa hii miji inayokua au inayoanza nayo ni vyema ukawepo mpango kabambe wa kuipima na kuipanga kwa ajili ya mwonekano endelevu kuelekea mji au jiji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa sasa hivi miji inakuwa changanyikeni na kutokuwa na miundombinu, kwa mfano Sumbawanga, Kigoma, Tabora, Mpanda na kadhalika, hivyo matumizi bora ya ardhi iwe ni zoezi kwa vitendo kila eneo la hapa nchini na kufanyiwa tathmini kwa
kipindi kifupi ili kuleta ufanisi na matokeo ya kuonekana na kusonga mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, migogoro ya wananchi na hifadhi, wafugaji na hifadhi, wakulima na wafugaji sasa ni wakati wa kutokana nayo. Serikali ichukue hatua ya uthubutu kabisa wa kushughulikia tatizo hili la migogoro liweze kutoka ndani ya jamii yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara husika kwa namna moja au nyingine kukutana na wamekwishafanya hivyo ni vema wakatoa makubaliano yao ya utekelezaji mapema; kama ni kubadili sheria lifanyike; kama kuwekwa kanuni ziwekwe na kupitishwa; mpango wa matumizi bora ya ardhi kuwekwa kwenye sheria lifanyike na kama kufutwa kwa baadhi ya sheria zifutwe na kadhalika

Mheshimiwa Mwenyekiti, kucheleweshwa kwa taarifa ya kikao cha pamoja cha Wizara husika kwa Bunge ili kufanyia kazi na kurejesha kwa jamii kwa utekelezaji ni hatari. Ni vyema sasa tukakamilisha zoezi hili la kufuta au kupunguza migogoro na kujenga imani kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naunga mkono hoja.