Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.

Kwanza, napongeza taarifa zote mbili za Kamati, lakini nina concern mbili za msingi sana; ya kwanza, upande wa migogoro ya wafugaji, wakulima na hifadhi zetu. Naomba Serikali hili iliangalie kwa mtazamo wa hali ya juu sana. Migogoro hii inasababisha maafa, inasababisha matatizo makubwa sana na kila malalamiko ya Wabunge, hapa tunalalamika kila wakati, sasa naomba Serikali itusikilize. Wananchi kule wana matatizo, lakini cha msingi ni kwamba tunaomba kuwe na ushirikishwaji wa wananchi katika kuainisha mipaka hii na wananchi wapewe nafasi ya kuweza kushiriki katika maamuzi haya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, suala la mifugo kukamatwa hovyo hovyo, tunaomba Serikali iliangalie sana.

Tunawatia umasikini wananchi wetu. Tunaomba kama ni sheria, basi iweze kuangaliwa upya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine ni suala la uvuvi haramu. Hakuna ambaye anashabikia uvuvi haramu, lakini mtindo unaotumika siyo mzuri, unaumiza wananchi wetu. Leo tuna wananchi wanakuwa maskini; asubuhi tajiri, jioni maskini. Serikali ya CCM haisemi namna hiyo, wala Mheshimiwa Rais hasemi namna hiyo. Tunaomba Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana hii, hebu waonee huruma wananchi hawa, hawa ni Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais alikuwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, alianzisha utaratibu mzuri sana wa BMU. Leo hii wananchi wanalia, wanaililia Serikali yao, Mheshimiwa Waziri upo, tusaidie! Tena unatoka sehemu ya Kanda ya Ziwa, kitu ambacho ni aibu. Sasa wananchi tusemeje? Wabunge tumesema, tunakueleza Mheshimiwa Waziri, hutusikii. Tunaomba utusikie kwa hili kupitia Bunge hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tuweke azimio, ni namna gani iliyo sahihi zaidi ya kuweza ku-moderate suala zima la uvuvi haramu? Hatupendi, samaki hawana mpaka. Sisi bila kushirikisha nchi ya Kenya na Uganda, tunafanya kazi bure. Zoezi hili lazima liwe shirikishi la wadau wote wa Ziwa Victoria. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo hii tena ukienda Mwibara kwa Mheshimiwa Kangi wanalia, ukienda Musoma wanalia, Busega wanalia, Magu wanalia, Geita wanalia, kila mahali wanalia, Kagera wanalia na sisi tulie humu Bungeni? (Makofi)

Mheshimiwa Waziri naomba uwe msikivu, acha kiburi, kuwa msikivu. Sikiliza maneno ya wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.