Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

Hon. Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kuhusu shughuli za Kamati kwa mwaka 2017.

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi hii. Kufuatana na takwimu ni asilimia 75 ya wananchi wanategemea kilimo na kilimo chetu kinachangia asilimia mia moja ya chakula. Mwaka 2016/2017, sekta ya kilimo imekua kwa asilimia 1.7 na katika kipindi cha nusu mwaka yaani Desemba kilimo kimekua kwa asilimia 3.1. Ukuaji huu wa kilimo hauridhishi, inabidi Wizara na Serikali ifanye jitihada za kuwezesha kilimo kukua na kuweza kuwasaidia wananchi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ili kuwa na kilimo chenye tija ni bora kutumia kanuni bora za kilimo na kanuni bora za kilimo ni pamoja na kutumia pembejeo za mbolea, mbegu na kadhalika. Imekuwepo tabia ya wakulima kutotumia mbolea ya kutosha na mojawapo ya sababu ni bei kuwa ghali. Kwa mfano, hapa Tanzania wakulima wengi wanatumia mbolea kilogramu 10 kwa hekta ambapo kilogramu zinavyoshauriwa ni 90 kwa hekta. Kwa hiyo, nashauri hili jambo liangaliwe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishukuru Serikali kwa kuja na huu mfumo wa ununuzi wa mbolea kwa pamoja. Hata hivyo, naishauri Serikali iufuatilie mfumo huu kwa karibu kwa sababu umeanza kuwa na changamoto yake kwani viashiria vimeanza kuonekana. Kwa mfano, kuna maeneo katika Mikoa inayozalisha chakula kwa wingi mbolea hii haikufika kwa wakati. DIP ni mbolea ya kupandia na urea ni mbolea ya kukuzia sasa unapeleka DIP wakati mazao yameshakuwa haiwezekani kwa sababu DIP ni mbolea ya kupandia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali na Wizara kupeleka mbolea hii kwa wakati muafaka. Tulipopitisha kwenye Bunge lako hili Tukufu kuwa tuweze kununua mbolea kwa pamoja tulisema ni ili tuweze kupata mbolea kwa wingi na kila mdau aweze kupata mbolea ambayo anaitaka baada ya kufuta ile mfumo wa kutumia ruzuku ambapo ilikuwa inatoa mianya ya rushwa. Naomba Wizara ijitahidi ili kila mdau wa kilimo aweze kuipata kwa wakati na bei elekezi iweze kutumika kwa sababu mahali pengine mpaka sasa hivi hiyo bei elekezi haifuatwi bado bei iko juu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa niongelee upande wa maji vijijini na mijini. Bado tuna tatizo kubwa kwenye maji mijini pamoja na vijijini, ni asilimia 56 vijijini na asilimia 69 mjini. Kwa hiyo, nashauri kwa upande wa maji Serikali yetu iweze kutilia mkazo kuona ni namna gani tunaweza kupata maji ya kutosha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo cha umwagiliaji ni muhimu sana, lakini mpaka sasa hivi ni asilimia 1.6 tu ndiyo tunalima kwa umwagiliaji. Kwa namna hii hatuwezi kufika mbali kwa kilimo cha umwagiliaji na hatuwezi kusema kuwa tutakuwa na usalama wa chakula kama hatutatilia maanani kilimo cha umwagiliaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nasisitiza Serikali iweze kutoa hela za kutosha kwenye kilimo cha umwagiliaji. Kuna mabwawa, kwa mfano, Bwawa la Kidunda, usanifu wake ulifanyika tangu 2004 lakini pia kuna mabwawa mengi ya umwagiliaji ambayo mpaka sasa hivi hayajakamilika. Nashauri Serikali pamoja na Wizara tuweze kuona jinsi ya kukamilisha mabwawa haya kusudi tuweze kujikita kwenye kilimo cha umwagiliaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni fedheha ambayo imetokea kweli kwenye upande wa korosho. Naomba Wizara iweze kuangalia hiki kitu kichotokea cha korosho zetu kukutwa na mawe na kokoto huko Vietnam. Kwa hiyo, naomba nalo liangaliwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwenye wadudu waharibifu wa mazao kwenye Mikoa yetu hata Morogoro tuna tatizo la viwavijeshi…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)