Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

Hon. Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa nafasi ya kuweza kuchangia hotuba ya Mwenyekiti wa Kamati ya miundombinu. Kwanza nachukua nafasi hii kuwashukuru sana Wajumbe wote wa Kamati ya Miundombinu kwa taarifa yao nzuri kabisa ambayo imetupa mwongozo kama Serikali katika kutekeleza majukumu yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nawashukuru Wajumbe wote kwa ushauri mbalimbali ambao mmeendelea kutupatia ambao umetuimarisha katika kutekeleza majukumu yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa muda wenyewe siyo rafiki sana, nitajikita moja kwa moja kwenye suala la Mamlaka ya Viwanja vya Ndege. Tulipata maelekezo na ushauri mzuri sana kutoka kwa Kamati kuhusu namna ya kuweka mipaka kwenye viwanja vyetu ambavyo kwa kweli vinavamiwa. Nakiri ukweli kwamba viwanja vyetu vingi sana vinavamiwa na Watanzania aidha, kwa kujua au wakati mwingine kwa kutojua. Tumeendelea kuwasiliana na mamlaka zinazohusika kuhakikisha kwamba viwanja vyetu vinabaki salama.

Mheshimiwa Naibu Spika, nachukua nafasi hii kuwashauri Watanzania, kabla hawajafanya maendelezo ya sehemu yoyote waliyopata nafasi ya kiwanja karibu na Taasisi za Kiserikali ni vizuri sana wakawasiliana na mamlaka zinazohusika kabla ya kuweka maendelezo ya kudumu. Kwa upande wetu Serikali, sasa hivi tunajiandaa na tunatengeneza Kitengo maalum cha Real Estate kwa mamlaka ya viwanja vya ndege ambacho kitafanya kazi ya kufuatilia viwanja vyetu vyote kubaini mipaka yetu yote na kufuatilia kupata hati. Kwa sababu bila kutengeneza Kitengo hicho cha Real Estate tutapata matatizo kidogo katika kufuatilia hizo hati.

Mheshimiwa Naibu Spika, nizungumzie kidogo kuhusu Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA). Nashukuru sana kwa pongezi ambazo Kamati wametupatia, tunazipokea kama Serikali na tunakiri kwamba TCRA kwa kweli inafanya kazi nzuri sana kuhakikisha kwamba ina-regulate masuala ya mawasiliano hapa nchini.

Mheshimiwa Naibu Spika, naendelea kuishauri TCRA na tunaielekeza kabisa kwamba wale wamiliki wa ving’amuzi binafsi ambao wanatakiwa watoe channel za bure kwa Watanzania watekeleze. Kama hawatatekeleza kwa wakati unaotakiwa, basi TCRA ijipange kuwachukulia hatua stahiki ili Watanzania waendelee kupata huduma za free chanel kama leseni ya wale watoa huduma inavyowataka. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nitajikita vilevile kwa suala la TTCL. Kwanza nitoe shukrani za dhati kwa ushauri wa kuimarisha TTCL ambao umetolewa na Kamati. Tunawashukuru kwanza kwa hatua mliyoichukua ya kui- support Serikali katika uanzishaji wa Shirika la Mawasiliano Tanzania (TTCL). Tunawashukuru kwa jinsi ambavyo mmeendelea kuipigania iweze kuwa imara. Huo ni moyo wa kizalendo ambao kwa kweli sisi Serikali tunaunga mkono; na tunaishukuru sana Kamati kwa jinsi ambavyo mnaipambania TTCL.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi TTCL inatengeneza muundo wa shirika. Baada ya hapo shirika limeshafunguliwa kama Shirika la Umma. Hivi sasa inaendelea na shughuli za kimkakati. Kwa mfano, sasa hivi ninayo furaha kueleza Bunge lako Tukufu kwamba kuna mkakati ambao TTCL unaendelea nao wakishirikiana na TANROAD wa kuhakikisha mizani yote Tanzania inawekewa vifaa maalum au inaunganishwa na mkongo wa Taifa kuhakikisha kwamba malipo yote yanayofanyika magari yote yanayopita yanaonekana kuanzia Makao Makuu ya TANROAD na hata Wizarani.

Mheshimiwa Naibu Spika, kupitia mradi huu tunategemea kutekeleza kwa awamu mbili. Awamu ya Kwanza tumeanza na Vituo 19. Mpaka sasa hivi ninapoongea Vituo 14 vimeshaunganishwa na mkongo wa Taifa, ambapo kila gari inayopita inaonekana lakini ina uzito unaoongezeka unaonekana. Kwa maana hiyo, hata charge wanayochangiwa kikawaida inaonekana moja kwa moja kwenye mitandao.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunategemea kwa kutekeleza mradi huu, mapato ya Serikali hayatapotea, lakini ile human intervention tutaipunguza kwa kiwango kikubwa sana. Kwa sababu ni kweli kwamba kupitia kwenye mizani Serikali tumekuwa tukipoteza mapato. Njia rahisi kabisa ambayo tumeona ni ya kutufaa ni kuanzisha hii system ambapo TTCL wameonesha uwezo mkubwa sana katika kuitekeleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile mfumo huu utaweza ku-share na mifumo mingine ya TANROADS ambapo ni mifumo kama ya fedha, mifumo ya emails, hata rasilmali watu. Kati ya vituo hivyo tunaamini kabisa tutakapoingia awamu ya pili tutatekeleza na vituo vingine vitakavyofuata ili kuhakikisha kwamba mapato yote ya Serikali hayapotei kupitia mizani.