Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Naibu Spika, nipende kupongeza Kamati ya Nishati na Madini kwa taarifa na kwa utendaji ambao umepelekea kudhibiti mianya ya utoroshaji wa rasilimali yetu ya madini.

Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa kuiomba Serikali kuharakisha uchakataji wa gesi yetu ili iweze kupunguza shida ya nishati hii ambayo inasababisha ukataji miti holela na hivyo kusabisha uharibifu wa mazingira.

Mheshimiwa Naibu Spika,nishauri Serikali kuharakisha ulipaji fidia kwa wananchi mahali ambako miradi ya umeme inapita kwani imesababisha umaskini kwa jamii pale ambapo wameweka X na kushindwa kulipa hivyo kusababisha wananchi kushindwa kuendeleza.

Mheshimiwa Naibu Spika, nishauri Serikali kupunguza urasimu kwa wawekezaji wa miradi ya madini kwani kunawakatisha tamaa wawekezaji hao.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nishauri Serikali kuwawezesha wachimbaji wadogo wadogo kwa kuwapa hitaji la muda mrefu kwani wameshindwa kupata pato kubwa kutokana na vifaa duni wanavyotumia katika uchimbaji.

Mheshimiwa Naibu Spika, nishauri Serikali kuangalia kwa upya juu ya Shirika la TANESCO kwa kulipunguzia mzigo wa kufufua umeme, kusafirisha na kuuza kunakopelekea utendaji ambao ni mgumu na usiokuwa mzuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, nishauri elimu kwa wachimbaji wadogo ili kusaidia kuwezesha kuchimba kwa tija.

Mheshimiwa Naibu Spika, nishauri Serikali kulipa malipo ya TANESCO kwani inapunguza utendaji wa TANESCO.

Mheshimiwa Naibu Spika, nishauri Serikali kujenga matenki ya Serikali ya kupokelea mafuta ili kudhibiti kwa urahisi upotevu wa mafuta unaopelekea Serikali kukosa kodi halisi ya mafuta hayo.