Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu wachimbaji wadogo wadogo; taarifa ya Kamati, imejikita na kuonesha faida na hasara zilizojitokeza wakati pesa za ruzuku zinatolewa kwa hawa vijana na vikundi vyao. Bado naona kuna haja ya Serikali kuhakikisha inazisimamia pesa hizi za ruzuku kwa wanufaika wa ruzuku hizi na kuwapa semina za kutosha.

Mheshimiwa Naibu Spika, mfano tu Mkoa wa Katavi leo baadhi ya vijana (vikundi vya wachimbaji wadogo wadogo) katika machimbo ya Isula, Milomo, Kapanda, Ibindi, Mtisi, Kampuni na Stalika, vijana hawa hawajapata mafunzo na hivyo mikopo au ruzuku chache zilizopatikana walizitumia kwa matumizi yao binafsi.

Mheshimiwa Naibu Spika, uchache wa pesa ya ruzuku kwa wachimbaji wadogo wadogo, Kamati imeshauri iongezwe kwa usimamizi maalum.

Mheshimiwa Naibu Spika, mazingira na manyanyaso kwa vibarua wa wachimbaji wadogo wadogo; hawa wanafanya kazi katika mazingira magumu sana bila waajiri wao kuwapatia vitendea kazi vyenye usalama katika mazingira magumu. Je, Serikali ina wachukulia hatua gani wachimbaji hawa wanaoajiri hawa vibarua hususan katika machimbo ya Ibindi, Kapanda, Mtisi na maeneo mengine kama Isulamilomo?

Mheshimiwa Naibu Spika, vibarua hawa wananyanyaswa na kunyimwa mishahara yao na wakihoji kuhusu maslahi yao wanafukuzwa kazi kwa sababu wamehoji. Je, Serikali hii ya CCM imeshindwa kusimamia unyanyasaji huu kwa vibarua wa wachimbaji wadogo wadogo?

Mheshimiwa Naibu Spika, uchache wa utoaji wa leseni kwa wachimbaji wadogo wadogo, usumbufu wanaopata wachimbaji hawa wanapofuatilia leseni zao kuna urasimu mkubwa sana kupitia Maafisa Madini wa Wilaya na Mikoa pamoja na Kamishna wa Kanda wa Madini, ni kwa nini leseni hizi zinatolewa kwa usumbufu mkubwa na kusababisha wachimbaji hawa kushindwa kufanya kazi zao na kupelekea kuporwa machimbo yao kumbe wanacheleweshwa ili wanyang’anywe machimbo yao. Je, Serikali hamwoni kwamba jambo hili linakwamisha uchumi, nini mkakati wa Serikali wa kuhakikisha inaongeza watumishi wa madini ili kuondoa usumbufu huu wa gharama wachimbaji kusafiri kutoka wilaya moja kwenda wilaya nyingine, mkoa kwa mkoa, kufuatilia leseni zao. Maoni ya Kamati yazingatiwe pia.

Mheshimiwa Naibu Spika, umeme wa REA Vijijini, changamoto za umeme vijijini ni kubwa na kama Kamati ilivyoshauri Serikali ihakikishe inasimamia uwekaji wa umeme katika vijiji vyenye vipaumbele si kubagua vijiji na kuviruka baadhi ya vijiji hili jambo si sawa. Serikali iliangalie jambo hili kwa sababu upatikanaji wa umeme vizuri unapelekea uchumi kukua.

Mheshimiwa Naibu Spika, upatikanaji wa umeme katika Mikoa na Miji mfano, Dar es Salaam; mpaka sasa umeme Mkoa wa Dar es Salaam bado ni tatizo na Mikoa mingine kama Katavi, Mbeya na Rukwa bado tatizo ni kubwa. Je, Serikali haioni haja ya kuhakikisha Taifa linapata umeme wa uhakika, maji ya kutosha halafu ndio mjipange kwa ajili ya mabadiliko ya uchumi wa viwanda, Je, Serikali haioni kuwa mnafanya kiini macho kuelekea uchumi wa viwanda?