Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

Hon. Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nichukue nafasi hii kushukuru kupata nafasi hii ya kuongea. Naomba niseme neno dogo kidogo, hata unapoamua kumnyonga mnyonge lakini mpe haki yake. Serikali ya Chama cha Mapinduzi Awamu ya Tano inafanya kazi nzuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tuzungumze kwa takwimu, tuwe tunazungumza kwa takwimu. Kwanza nazungumzia Kamati ya Nishati na Madini, nazungumzia upande wa madini sasa. Serikali ya Awamu ya Tano ya Mheshimiwa Rais Magufuli imefanya mambo makubwa mawili na mambo haya yamewavutia Madiwani wengine wanakuja wenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la kwanza kudhibiti madini yasipotee na jambo la pili ni upande wa ukusanyaji wa pesa za madini. Serikali ya CCM ya Awamu ya Tano kwa kipindi hiki cha mwaka 2017/2018 nusu tu tuhatujafika mwaka 2018, Serikali imekusanya asilimia 80.4 ya makusanyo ya mwaka mzima. Lengo ilikuwa mwaka 2017/2018, Serikali ikusanye bilioni 194.397 hadi Mwaka 2018 Desemba lakini Serikali hii imekusanya bilioni 156.311 sawa na asilimia 80, sasa utasema hiyo Serikali inacheza? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, msiwasikilize hawa, tumewazoea, sisi tunaangalia kazi inayofanywa na wananchi angalieni vizuri Serikali ya Awamu ya Tano inachapa kazi. Ningeshangaa sana Serikali inavyochapa kazi iungwe mkono na hawa, ningeshangaa, lazima hawa wakasirike. Kwa hiyo, msipate tabu Waheshimiwa Wabunge, twendeni kazini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, twende kwenye suala la REA, nipongeze Bunge la Kumi ndilo lilikuja na hii tozo ambayo imeleta manufaa kwa nchi yetu. Naomba nikubali kwamba jambo lolote linapoanza lina changamoto, huwezi kuanza jambo mara ya kwanza ukalifanya kwa asilimia 100, mara ya pili ukalifanya asilimia 100, kidogo kidogo REA itasimama. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitoe takwimu, mwaka 2008 umeme vijijini ulikuwepo kwa asilimia 2.2 tu kabla ya kuwa na REA. Ilipofika 2015 umeme vijijini ukafikia asilimia 21.02, hayo ni madogo jamani? Serikali inachapa kazi, sasa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2015 mpaka Desemba, 2017 angalieni Serikali ya Awamu ya Tano inavyochapa kazi, umeme vijijini umefikia asilimia 49.5. Sasa najiuliza hivi hamuyaoni hayo, wenzetu mna macho gani, tafuteni miwani. Serikali inachapa kazi jamani Wabunge wa CCM tujivune. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri Subira Mgalu, anajitahidi sana. Wiki iliyopita alikwenda Kilimanjaro, nampongeza sana, kuangalia matatizo yaliyotokana na REA I na REA II. Kwa hiyo, Serikali inafahamu kwamba kuna changamoto, alikwenda Mwanga, Rombo na akaja Same.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimemshangaa, Kata ya Vulha, Kata ambayo Mawaziri wachache sana wanafika, amefika Subira. Kule kuna mradi wa REA II, nilipambana nayo sana ile, Serikali ikapeleka umeme kule lakini haikumaliza. Mheshimiwa Waziri amekwenda kuangalia na amekwenda kuwahakikishia wananchi kwamba REA III inakwenda kumalizia, Serikali inafanya kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa Waheshimiwa Mawaziri, Waziri wa Nishati pamoja na Naibu Waziri mlikwenda Kilimanjaro lakini kuna Wilaya ina matatizo sana naomba nisimame hapa niiombee umeme kule ambapo haujafika, Wilaya ya Siha. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Siha kuna Kata moja ambayo ina vijiji vinne, hiyo Kata inaitwa Donyomurwakna. Kuna vijiji vinne kwenye kata hii, vijiji viwili vina umeme na vijiji viwili bado umeme haujafika. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niseme kitu kimoja, waacheni hawa, hakuna Serikali ambayo inaweza ikafanya mambo yote kwa wakati mmoja, haipo duniani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, naiombea Wilaya yangu ya Siha kwamba vile vijiji ambavyo Mheshimiwa Waziri nimekuletea kimaandishi uhakikishe vinapata umeme na Alhamisi ya wiki hii nahamia Siha. Naomba Watanzania wawe na uhakika kwamba Siha litakuwa Jimbo la Chama cha Mapinduzi.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwahakikishe Watanzania kwamba CCM inashinda Siha. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja, ahsante sana.