Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

Hon. John Wegesa Heche

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tarime Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa nafasi hii ya kuchangia ili niweze kusema kidogo kuhusu hoja zilizoko mbele yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kati ya matatizo makubwa ambayo nchi yetu imekuwa ikikabiliwa nayo ni ufisadi mkubwa unaolelewa na Serikali hii ya CCM. Ufisadi huu umekuwa kwenye miradi mbalimbali ya Serikali na kila mipango inayopangwa ukiangalia ndani yake unakuta kuna mkono wa kifisadi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mwaka 2010 mpaka mwaka 2013/2014, kulikuwa na msukumo mkubwa sana kuhusu suala la gesi kule Kusini. Msukumo wa hali ya juu kweli kweli, wananchi kule wakapigwa, wakawekwa ndani, likapelekwa mpaka Jeshi, watu wakawa tortured kwelikweli. Wakati ule hapa Bungeni kikaingizwa kitu tunaambiwa kwamba sasa tunataka ku-shift kutoka kutumia umeme wa hydropower tunakwenda kwenye umeme wa gesi.

Mheshimiwa Naibu Spika, hiyo ni Serikali ya Kikwete na ilikuwa ni mipango ya Serikali ya Kikwete. Watu wakalazimishwa kule likajengwa bomba pesa zikakopwa kwa walipa kodi maskini wa nchi hii wakawekewa kitu kwa kubambikiwa. Wananchi wa Kusini hawakukubali lakini mkatumia nguvu nyingi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo baada ya miaka mitatu, minne tume-shift tena tunaambiwa sasa tunakwenda kwenye Stieglers Gorge. Serikali iliyoingia hii sasa na yenyewe inatafuta jinsi ya kupiga, tutapigia wapi, sasa tupigie kwenye Stieglers Gorge. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, bomba la gesi lililojengwa kwa gharama kubwa kweli kweli matumizi yake tumeambiwa kwenye Kamati ni mpaka sasa ni asilimia sita tu peke yake na tuliaminishwa na Watanzania wakaaminishwa kwamba sasa hatutaki tena kutumia umeme wa maji kwa sababu is not anymore reliable. Sasa umeme unaoaminika ni umeme wa gesi.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa Serikali hiihii, ya Chama kilekile, Rais aliyeko ndiye alikuwa Waziri kwenye Serikali hiyohiyo, alikuwa kwenye Baraza la Mawaziri linalopanga mipango, leo amekuja anatuambia sasa tunaenda Stieglers Gorge. Stieglers Gorge haijawahi kuingia kwenye bajeti. Ukisoma kitabu cha bajeti cha mwaka jana hakuna kitu tulichojadili kuhusu Stieglers Gorge. Hakuna pesa zilizopangwa kwa sababu Bunge hili ndilo lipo kwa niaba ya wananchi kupanga mipango na ku-authorize matumizi ya pesa kwa niaba ya wananchi wa nchi hii ambao ndiyo walipa kodi. Bunge hili halikuwahi kupanga hicho kinachoitwa Stieglers Gorge. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sawa ni mradi mzuri na wote tunautaka, lakini kama tuliwekeana utaratibu na kama mwaka juzi tu tumechukua pesa za walipa kodi tukapeleka kwenye bomba, kwa nini tusi-utilize bomba kwa matumizi ya asilimia mia moja kabla hatujahamia kwenye hiki kinachoitwa Stiglers Gorge? Kama siyo kwamba kuna wingu la kaufisadi kapya kanatengenezwa hapa kwa sababu ufisadi uliokuwepo sisi hatukugusa? Kwa nini leo tunachukua pesa wakati bomba hili tunalitumia kwa asilimia sita peke yake? (Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nafikiri ni lazima Serikali ije hapa na majibu, iwaambie Watanzania kwamba gesi tuliyowaaminisha miaka miwili, mitatu, iliyopita kwa Serikali hii hii ya Chama kilekile ni nini kimeikumba gesi. Kwa nini gesi inatumika kwa asilimia sita na sasa tunahama tena kurudi kwenye hydro ambayo tuliwaambia wananchi kwamba haiko reliable kwa sababu mvua zetu haziaminiki.

Mheshimiwa Naibu Spika, hili bwawa tumeambiwa juzi kwenye semina tarehe 3 lina urefu wa kilometa 100 yaani kama unatoka Chalinze mpaka Dar es Salaam na upana wake ni kilometa 25. Mimi ninachotaka kutoka hapa Waziri atuambie hizo pesa ambazo angalau wamefikiria kwamba wanataka kuzitoa kwa ajili ya ujenzi wa hili bwawa, wanakadiria kutoa shilingi ngapi na kwenye bajeti ipi na waliipitisha wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu wamesema within three months tayari kutakuwa na mobilization inafanyika pale kwa ajili ya kuanza kujenga bwawa. Sasa huyo aliyewapitishia hizo hela ni nani? Nani anatoa mamlaka ya pesa nyingi hizo kupitishwa kinyemela hivyo bila Bunge hili? Ni nini kazi ya Bunge hili ambalo wananchi maskini kila siku wanatoa kodi, wanajinyima kwelikweli, mama zetu hawawezi hata kununua vidonge lakini wanalipa kodi kutulipa sisi mamilioni ya pesa tukae hapa tujadili mipango yao na hatufanyi hiyo kazi, tuna haja gani ya kuendelea kuwa hapa? Tunataka Waziri atuambie. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tuje kwenye REA. Mwaka jana tulizindua kitu kinaitwa REA wakaja wakandarasi na Naibu Waziri wakati ule sasa hivi Waziri rafiki yangu kweli, tulikuwa naye pale Bunda. Wakaja wakandarasi wakatuaminisha kwamba kufikia Desemba, kwa mfano, miradi ya densification, Waziri ni rafiki yangu na yeye yuko hapa atathibitisha ninachokisema, kwamba densification Desemba umeme unawaka. Kwanza ilikuwa Oktoba baadaye ikasemekana sijui imekuwaje Desemba.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo tunazungumza maeneo kwa mfano ya Sirari kwenye mji ambao una population ya watu 45,000, hawana umeme pale. Hata mradi wa densification wenyewe tulioahidiwa hakuna kitu wala hakuna hata nguzo zilizopelekwa mpaka sasa hivi mradi tulioambiwa Desemba utakuwa umewaka. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hizi pesa za REA Mheshimiwa Waziri ziko wapi? Kwa sababu hizi pesa siyo za bajeti wala sio za nini, ni pesa za walipa kodi maskini ambapo kila siku tunanunua petrol tunakatwa Sh.50. Mama kijijini kule akinunua mafuta ya taa mnamkata pesa au hizi pesa tena mnachukua mnaenda kununulia Madiwani wakati hizi pesa zinatakiwa zilete umeme? Zinaenda wapi pesa ambazo ziko ring-fenced? Pesa ambazo zinatolewa kabisa zikiwa na matumizi, mtu anaenda kununua mafuta anajua matumizi yake ni kwamba zituletee umeme wa REA, ziko wapi na ni kwa nini haziendi kwenye REA? Nataka Waziri atuambie hizo pesa ziko wapi? (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, leo wamesema TANESCO inadaiwa na sisi wote ni wajumbe tunajua TANESCO inadaiwa. TANESCO hiyo ambayo inadaiwa iko hoi, wameenda tena kubomoa na jengo lake linalokadiriwa kufikia bilioni 54, sijui ni la kwake au walikuwa wamepanga au nini. Yaani mgonjwa ambaye yuko mahututi kwelikweli anaweza kufa sasa wamenyang’anya hadi sehemu ya kulala ananyeshewa na mvua. Sasa hawa hivi mipango yao ni ipi? Ni kwenda mbele au wanaenda mbele hatua mbili, wanarudi kumi na tano nyuma wanajipongeza? Kwa sababu sasa hivi wamedhibiti vyombo vya habari, wanadhibiti hata Wabunge kuongea, wakiongea tu wanashughulikiwa yaani wao wenyewe wanajifungia wanafanya maamuzi ambayo miaka mitatu ijayo mbele au kwa sababu wanajua mwaka 2020 hawarudi sasa wanataka tukiingia Serikalini tusikute chochote hapa. (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sababu kama leo wanakwenda kukopa kwenye benki za kibiashara kuwekeza kwenye mradi mkubwa kama wa Stieglers Gorge wanalipaje hizi pesa? Kama siyo kwamba wanataka Serikali itakayokuja ishindwe kufanya kazi yake?