Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

Hon. Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 na Kamati ya Kudumu ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017.

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Ahsante sana Mheshimiwa Naibu Spika, nami kwa kunipatia fursa hii niweze kutoa nami maoni yangu, nami pia ni mjumbe wa Kamati, mengi tumeshayachangia kwenye Kamati; na yale mazuri pia tuliyoishauri Wizara na Serikali pia wayachukue kwa mustakabari wa Wizara ya Nishati na Madini.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumeona haya mambo yanavyokwenda katika hii Wizara na hii Wizara haijawahi kumuacha mtu salama. Tumeona migogoro mingi ambayo imetokea kwenye hii Wizara ya Nishati na Madini, mpaka Mheshimiwa Rais akachukua jukumu la kutenganisha hizi Wizara zikawa Wizara mbili.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuna mambo mbalimbali ambayo yamefanyika kwenye Kamati hizi. Tumeona yale masuala ya makinikia, mambo ya michanga yalivyokwenda, sasa Watanzania wengi bado wanahoji pia wanataka angalau wapate taarifa kile ambacho tulikuwa tunakidai kiko wapi na ni kitu gani tulichonufaika nacho mpaka sasa hivi. Si vibaya sana tukitoa taarifa tukawaambia Watanzania kama kipindi kile tulivyokuwa tumewashirikisha namna tulivyokuwa tunaibiwa kwenye masuala ya migodi. Kwa hiyo, niiombe Serikali na Wizara itoe taarifa ili wananchi wajue ni kiasi gani tulichokipata mpaka kwa sasa hivi kwa suala lile la mchanga. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna hili suala la wachimbaji wadogo wadogo; hawa wachimbaji wadogo wadogo huwa kuna wachimbaji ambao wanapatiwa ruzuku na Serikali. Lakini umeangalia katika suala letu la taarifa ilivyotoka umeona ni namna gani ni wachimbaji wachache sana ambao wamepata ruzuku ya Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, niishauri sana Serikali na Bunge lako Tukufu kuhusu hii Serikali ya wachimbaji wadogo wadogo, tuangalie humu ndani kwa kina hizi pesa zimekwenda wapi, huku tukianza kuangalia tukichimbua kwa kina kuna vitu vingi sana vimefichika huku kwa wachimbaji juu ya hizi ruzuku zilizotolewa kwa Serikali kwa ajili ya kuwafikia wachimbaji wadogo wadogo. Umeona ni namna gani wamepata wale wachimbaji, waliopata ni watatu. Sasa tuangalie zile pesa ambazo zilikuwa zimetengwa kwa ajili ya wachimbaji wadogo wadogo hizi fedha zimekwenda wapi? Na kama zimeishia kwenye mifuko ya watu au kama watu wamepiga deal basi naomba haya masuala yafuatiliwe kwa kina zaidi ili tuzidi kugundua huu uozo ambao uko kwenye Kamati ya Madini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu GST, hawa ni wataalam na endapo tungekuwa tumewatumia vizuri hata hawa wawekezaji wanaokuja kwa kweli wasingeweza kuvamia maeneo kabla hawajapata utafiti.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tuangalie hii bajeti ambayo tunaitenga katika hii Wizara, hizi taasisi zinafikiwa au zinapelekwa kwa wakati? Sasa kama vitu kama hivi hawa GST hawawezeshwi kwa wakati, sasa tuangalie ni namna gani hii Wizara tuwawezeshe hawa GST kabla wachimbaji hawajaenda kuvamia maeneo wafanye kama utafiti kama kweli huko wanakoenda kuchimba kuna madini au wanaenda kufanya uharibifu wa mazingira. Hata kama wawekezaji wamekuja hawa wafanye kwanza utafiti wa kutosha na waangalie pale kuna madini kiasi gani ili waruhusu wawekezaji sasa nao wachimbe yale madini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuangalie wataalam ni namna gani Serikali sasa mnaweza kuwapa kipaumbele ili tuangalie tunadhibiti haya madini tunayosema tumeibiwa kwa siku nyingi yawanufaishe Watanzania kwa ujumla.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuna mambo mengi sana kuhusiana na masuala ya REA. Niipongeze Serikali kwa haya masuala ya REA, lakini bado kijijini kuna tatizo sugu sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, umeme unapotolewa utakuta wale wafanyabiashara au mtu ana shule yake, au mtua ana uwezo, basi wanaruka vijiji vya wale watu ambao hawana uwezo. Niombe hao watu wakusanywe kwa pamoja umeme kama unapita usibague huyu ana uwezo,
huyu hana uwezo, ili wapate wote kwa wakati muhafaka hayo yanatotakiwa kwenye umeme wa REA.

Mheshimiwa Naibu Spika, tuje kwenye madeni ya TANESCO. Hili Shirika limekuwa likijiendesha sana kwa hasara, kama ulivyoona tulivyotoa maoni yetu kwenye Kamati yetu. Tuangalie na hawa wadaiwa sugu wanachukuliwa hatua gani na Serikali ili wapate kulipa. Hata kama ni taasisi za Serikali basi tuhakikishe ni namna gani wanarejesha haya madeni TANESCO ili TANESCO iweze kujiendesha.

Mheshimiwa Naibu Spika, hii Kamati yetu tumechambua mambo mengi mazuri yaliyoongelewa humu kwenye Kamati, naomba yachukuliwe, lakini sana sana pia niende kwenye suala la barabara. Kuna barabara hizi ambazo tumekuwa tukizijenga, lakini barabara hizi tunazijenga kwa gharama kubwa halafu zinaharibika kwa muda mchache. Sasa niulize Serikali hawa wakandarasi wanaohusika na hizi barabara wanachukuliwa hatua gani endapo zile barabara zinaharibika kwa kipindi ambacho ni cha… na watoe guarantee kama hizi barabara wanazozijenga zitachukua muda gani, na zikiharibika kabla ile guarantee haijaisha basi wachukuliwe hatua.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia tuangalie suala la bandari. Tuangalie bandari hizi bandari bubu ambazo ni tatizo, kuna vitu vingi sana vinapita kwenye bandari bubu. Sasa tunazidhibiti vipi hizi bandari bubu ili tuache kupitisha, ziache kupitisha mizigo, vitu vya haramu na mambo mengine ili wale ambao wanakwepa kodi nao wadhibitiwe ili zile kodi zirudi Serikalini.

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na suala Bandari ya Dar es Salaam kwenda Zanzibar bado kuna malalamiko sana kwa wafanyabiashara ambao wanatoka Zanzibar. Kumekuwa na changamoto kubwa sana kwenye suala hili la wafanyabiashara wa Zanzibar. Unakuta umelipia mzigo wako Zanzibar, ule mzigo ukifika tena pale bandarini unakuwa-charged ushuru. Unakuta umetoka na kiporo (mfuko) chako kidogo, labda ni kiporo cha mchele au vitu vyako vidogo vidogo umenunua unapeleka Zanzibar, kwa hiyo ukifika pale unachajiwa ushuru. Sasa tuangalie ni namna gani ili suala la Muungano kuhusu masuala ya bandari ni namna gani sasa tuliweke ili pande zote mbili zinufaike, upande wa Zanzibar wasilalamike na upande wa Tanzania Bara usilalamike. Tusiwe kule tumeshalipa kodi wakija tena huku wanalipa kodi.