Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru. Awali ya yote niwashukuru Wajumbe wa Kamati zote tatu wakiongozwa na Wenyeviti wao kwa taarifa zao nzuri hasa kwa maelekezo na ushauri tutauzingatia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla sijaenda mbali nirekebishe kidogo tafsiri ambayo siyo. Mheshimiwa Mbunge nadhani alikuwa anasherehesha, aliyesema Serikali haijafanya lolote kwenye zao la korosho lakini mwisho akakiri kwamba labda kutafuta bei. Katika biashara ya uchumi kinacho-drive kila kitu ni bei. Panga bei nzuri watu watahangaika wenyewe. Kwa hiyo, nadhani alikuwa anasherehesha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nijibu kidogo hoja zilizozungumzwa lakini nimjibu na mchangiaji mmoja Mheshimiwa Mbunge aliyetafsiri taarifa za wepesi wa kufanya shughuli. Zile takwimu alizoziangalia aende akaangalie na distance to frontier. Distance to frontier inakueleza unapokuwa umepata maksi mbaya ujiangalie wewe ni wa ngapi katika yule aliyekutangulia. Ukiona upo above 50% hupaswi kulala bila usingizi, nakubali hatufanyi vizuri na pale ambapo hatufanyi vizuri tumejitathmini na tumeandika andiko ‘The Blue Print’ maeneo yote yenye matatizo tutayakosoa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna mtu ambaye anaweza kukaribisha wageni halafu wageni hao unashindwa kuwawekea kiti au namna ya kuwakirimu. Namna ya kuwakirimu wawekezaji ni kuwatengenezea mazingira mazuri ya kufanya biashara. Mimi binafsi nakiri kwamba ninapopataka siyo hapa, nitaendelea kuhimiza kwa kushirikiana na wenzangu tuweze kwenda kwenye nafasi nzuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie suala la viwanda vilivyobinafsishwa. Siyo mapenzi ya Waziri mwenye dhamana wala mtu yeyote ni Ilani ya Chama inasema viwanda vilivyopo sasa vifanye mpaka ukomo (maximum capacity), viwanda vilivyobinafsishwa vyote vifanye kazi na tuhamasishe viwanda vingine vije. Kwa hiyo, orodha ya viwanda vilivyobinafsishwa kama alivyozungumza Comrade Lusinde nitaileta hapa Bungeni mje muione, kazi inafanyika lakini ngoja niwaambie, viwanda vile lazima vifanye kazi, kama huwezi kufanya kazi mpe mwenzako na tutakapofika wakati wa factoring unaweza kushtakiwa kwa uhujumu uchumi na dhamana yake mnaifahamu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ulinzi wa viwanda. Tunalo jukumu la kulinda viwanda na viwanda tunavilinda kwa ngeli mbili, moja ni kuangalia mpangilio wa kodi katika maeneo ya kikanda tulipo. Bado hilo zoezi linaendelea hatujafanya vizuri na Kenya wanajua kututegea kwenye suala hilo na tunalijadili Serikalini tutahakikisha kwamba hatupangi bei ambazo majirani zetu wana-take advantage, hilo tutalishughulikia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili ambalo tunakiri upungufu katika shughuli hiyo ni tatizo la under valuation na under declaration na smuggled items. Tunalijua na tutalishughulikia na tutalifanya kazi. Kama alivyosema Comrade Lusinde watu wanaouza hivi vinywaji katika chupa za plastiki kumbe tatizo siyo chupa za plastiki, tatizo ni kuuza katika chupa za plastiki chini ya ujazo uliokubalika. Tatizo la pili ni kuuza bila kuweka ile stampu ya TRA. Kwa hiyo, wale ni

majambazi kama majambazi wengine, naomba mkiwaona mniambia mimi au mwende Polisi mtafute RB. Ulinzi wa viwanda ni jukumu la sisi wote sio jukumu la Serikali peke yake au Waziri mwenye dhamana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kidogo mkakati wa kuendeleza viwanda. Mkakati wa kuendeleza viwanda upo ni Integrated Industrial Development Strategy lakini tumezungumza ni viwanda gani tunavitaka, tunataka viwanda vile ambavyo vinaajiri watu wengi, tunataka viwanda vile ambavyo vinachakata malighafi za wananchi, tunataka viwanda vile ambavyo bidhaa zake zinatumika kwa wingi na imekuja kwa maelekezo ya Mheshimiwa Rais tutengeneze viwanda vitakavyochakata mali za asili ambazo tulipewa kipekee na Mwenyezi Mungu. Ndiyo maana ukuta unajengwa pale kuzunguka Tanzanite. Hivyo ndivyo viwanda tunavyoshughulikia, tumefanya vizuri katika hilo. Jukumu la Serikali ukisoma Mpango wa Pili wa Miaka Mitano ni kuhamasisha sekta binafsi iweze kuwekeza, tunajitahidi, tunafanya kazi vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mtu asije akadhani kwamba sisi hatujafanya kazi na mambo yote haya yanajulikana tatizo ni mapenzi ya kufika finally wakati ndiyo mchezo unaanza. Tunajenga viwanda na tunategemea come 2025 itakuwa nchi ya uchumi wa kati tukiwa na viwanda, leo ndiyo mwaka wa pili na niliambie Bunge lako kwamba kwa kipindi cha miaka miwili viwanda 3,306 vinafanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania tuna installed capacity ya saruji 10.9 millions tans wakati matumizi yetu ni
4.8 millions tans. Tanzania tunazalisha vigae Kiwanda cha Mkuranga square 80,000, Kiwanda cha Chalinze kinazalisha 50,000, ukienda Rwanda ukipeleka kigae cha China hawanunui wanataka vya Tanzania. Kwa hiyo, msidhani kwamba tuna hali mbaya, tunataka kuwa mbele lakini hapa tulipo hatupaswi kujinyonga kwa sababu hatufanyi vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kasi ya utendaji wa miradi ya Serikali. Imetolewa hoja kwamba miradi ya Serikali inakwama, ndiyo, tumelizungumza hapa suala la PPP, tumezungumza hapa suala la hizi sheria kuna upungufu na hayo yote hayo tumeyaona na tunayafanyia kazi. Kwa sababu tukienda bila kuyarekebisha haya na kuyaleta mbele ya Bunge tutakuja kuulizwa tulifanya nini. Tunayafahamu haya, tutayarekebisha ikiwemo suala la Kurasini Logistics Centre na General Tyre.

Mheshimiwa Mwenyekiti, General Tyre tunajua tunataka kufanya nini, lakini sheria sasa inayokuwezesha namna ya kushirikiana na yule private sekta ndipo inapokuja ngoma. Taasisi zinazohusika, watendaji wa Serikali wanashughulikia suala hili ili tuwe na mwendelezo mzuri wa kuweza kufanya shughuli hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, muda siyo rafiki, nakushuru na naomba kuunga mkono hoja.