Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Mary Deo Muro

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. MARY D. MURO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapenda kupongeza Kamati ya Uwekezaji Mitaji kwa taarifa ambayo inaeleza hali halisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa kuchangia juu ya Shirika la Elimu Kibaha (KEC) ambalo lilianzishwa kwa ajili ya shamba darasa kwa ajili ya wananchi kujifunza maendeleo mahali pale. Ningependa kusema kuwa tunapoangalia Shirika la Elimu Kibaha tulishuhudia uendelezaji wa shirika hilo huko nyuma miaka ya themanini lilikuwa na viwanda vya kutotolesha vifaranga na ufugaji wa ng’ombe ambao sasa hivi haliko hivyo na limekufa kabisa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niishauri Serikali kuangalia taasisi hii ambayo ilikuwa na shule, Chuo cha Maendeleo kilichokuwa kinafanya shamba darasa na kutoa vijana kwenda kujiajiri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kushauri Serikali kuharakisha uundaji wa Bodi ya Wakurugenzi wa RAHCO, kampuni hodhi ya rasiliamli za reli. Nimeona niseme hivi kwani ni wakati ambao sasa tunatengeneza Reli ya Standard Gauge na kampuni hii haina bodi ya rasilimali hiyo itakuwa shida. Niishauri Serikali iharakishe uundaji wa bodi hii ili iweze kusimamia rasilimali za reli kuweza kuleta ufanisi wa uendelezaji wa reli nchini.