Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Rhoda Edward Kunchela

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Katavi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. RHODA E. KUNCHELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kutolipa madeni kwa wakati katika Mashirika ya Umma. Ukipitia Taarifa ya CAG kwa ujumla katika maeneo mengi CAG ameshindwa kutembelea baadhi ya maeneo kwa sababu ya ukosefu wa pesa katika Ofisi yake. Ninaomba Serikali ilipe madeni ili tupate taarifa za kimahesabu kutoka katika Ofisi ya Ukaguzi na Serikali ijikite kulipa madeni ili tuendeshe kazi za wananchi waliowalipa kodi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ilipe madeni ya DAWASCO, Jeshi, TANESCO na maeneo mengine ambayo Serikali hii imeshindwa kuyalipa kwa wakati na kusababisha taasisi za Serikali kushindwa kujiendesha zenyewe na matokeo yake taasisi hizi zimekuwa zikijiendesha kwa hasara na mikopo pia. Ni kwa nini Serikali inashindwa kulipa madeni hayo kwa wakati na huku mwananchi wa kawaida, mfano anadaiwa na Idara ya Maji 5,000/= tu anakatiwa maji. Je, hamuoni kwamba, Serikali inashinwa kujisimamia yenyewe kupitia taasisi zake? Ni lini sasa Serikali itaanza kulipa madeni haya makubwa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ya Sheria ya Manunuzi ya Umma. Katika mfumo wa manunuzi nimeangalia mambo makuu mawili ambayo kwa upana wake Serikali iangalie namna ya kuboresha au kurekebisha sheria. Sheria hizi za manunuzi zinasababisha mchakato wa manunuzi kununua mali za Serikali kuchukua muda mrefu, mchakato wa kutangaza tenda unakuwa mrefu sana, lengo ni kupata (Supplier) mwenye vigezo, lakini Serikali ione namna ya kuziangalia sheria hizi kimfumo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto ya muda; Miradi kusimama kwa sababu tu vifaa vimechelewa kutokana na manunuzi kuchukua muda mrefu. Changamoto ya gharama, masuala ya manunuzi yanasababisha pia, Serikali kununua bidhaa kwa gharama kubwa na kwa baadhi ya watumishi wasio waaminifu wamekuwa wakipata 10 percent na huku wakiibia Serikali kupitia mfumo huu wa manunuzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Ziara za Ukaguzi wa CAG na Bunge. Kwa ujumla malalamiko yaliyopo ni CAG kushindwa kufanya ukaguzi katika baadhi ya maeneo nchini na Bunge kupitia Kamati zake pia, zimeshindwa kukagua miradi. Dhamira ya uwazi wa pesa ya umma iko wapi? Au Serikali inafanya maksudi kunyima ofisi ya CAG pesa?