Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Sixtus Raphael Mapunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. SIXTUS R.MAPUNDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kunipa nafasi na mimi ili nichangie jioni ya leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, niseme kwa masikitiko makubwa kwamba natoa pole kwa familia ya Mzee wetu Kingunge Ngombale Mwiru, ambaye ndiye alikuwa Mwalimu wetu sisi vijana wa siasa na amewahi kuwa Katibu Mkuu wa TANU Youth League na mwasisi wa Umoja wa Vijana wa CCM; kwa namna ya pekee sana natoa pole zangu sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Baada ya hizi pole naomba nijielekeze sasa kwenye kuchangia kwenye hotuba zilizowasilishwa leo hapa Bungeni. Umuhimu wa mashirika na taasisi za umma kwa nchi yetu ni mkubwa sana. Mashirika mengi yalianzishwa kwa lengo moja, kwa kutoa huduma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo la pili ni kutoa gawio kwa Serikalil; huo ndiyo ulikuwa moyo wa sprit behind ya kuanzisha haya mashirika. Kwa bahati mbaya ufanisi wa mashirika hayo yote hauwezi ukapimika kwa faida wanazotoa au hauwezi ukapimika vizuri na ukaonekana kwa aina ya huduma wanazozitoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na hoja hiyo niiombe Serikali iyatazame haya mashirika na kuyasaidia kulingana na aina ya huduma au matokeo ambayo Serikali inatarajia. Huwezi ukalipima shirika linalotoa huduma kwa jamii kwa vigezo vya faida lakini huwezi ukalipima shirika ambalo unatarajia linaendeshwa kibiashara one hundred percent kwa vigezo vya huduma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika ujumla wake performance indicators ni kipimo muhimu kwa kupima ufanisi wake. Nimelitizama kwa kina sana shirika la ATCL niombe Serikali iitizame ATCL katika jicho la tatu. Ukilitizama kwa kiasi gani linaleta faida na kiasi gani liko efficient unaweza usipate jibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe Serikali sasa ingalie na kuisaidia ATCL kwenye kipimo kingine ambacho kinaitwa spillover effects indicator au positive externalities indicator au a third party effect indicator. Hiyo ikoje; unaweza ukawa na shirika kwa nature yake jinsi ilivyo mpaka Yesu anarudi ukipiga pale ulichokiweka naulichokipata ndani ya lile lile shirika moja kwa moja usione faida, lakini likawa na faida nyingi sana zisizoonekana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye ATCL serikali msitegemee faida mtapata mwaka huu, mwakani au mwaka wa kesho kutwa, linaweza likanyumba katika nchi zozote itakazoelezeka lakini ATCL ina faida kubwa sana, kwanza ndiyo brand ya Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata hivyo, ATCL inasaidia sekta nyingine zikimbie, zikue na zilete faida kwa Taifa. Wanakwambia principal ya faida ya duniani kote inatokana na speed ya mtu anavyo-move kutoka hatua moja kwenda hatua nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfanyabiashara yeyote duniani asingependa kukaa masaa mengi barabarani, kwa jinsi anavyofika kwenye huduma kwa urahisi ndivyo faida inavyopatikana kwa hiyo niiombe Serikali iitizame ATCL na wala isiache kununua ndege kwa sababu tulishaona kwenye mashirika mengine kama Ethiopian Airline wamenyumba hawakupata faida, lakini hawakuacha kununua ndege na wamenunua ndege. Emirates hawajawahi kupata faida hawajaacha kununua ndege na wameongeza ndege nyingine kubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Air Rwanda wameongeza Mabombadia (Bombadier) na mamboing (Boeing) haya yote wanayofanya KQ mwaka jana waliyumba kiasi kwamba watu wakafikiri shirika litafungwa hawajaacha kununua ndege na wameongeza kununua ndege; kwa nini hawa wanafanya hivyo?

Mheshimiwa Mwenyekiti, wanafanya hivyo kwa sababu wanajua faida inayotokana na shirika hili siyo ya moja kwa moja ni ya huduma kwa upande mmoja, watu wata- move lakini kwa upande mwingine itasababisha sekta nyingine zikue hiyo ndicho wanachosema a third part effect indicator tunapaswa tuitazame katika lengo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine, Serikali imewekeza jumla ya shilingi trilioni 47.7 kwenye mashirika yote mpaka ilipofika Juni, 2017 lakini faida iliyopatikana kwenye investment ya shilingi bilioni 47.7 ilikuwa ni shilingi bilioni 8.2 tu ambayo ni sawasawa na asilimia moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama haya mashirika yangewekezwa vizuri na yakatengenezewa mazingira angalau yalete asilimia kumi tu ya investment ambayo tuliiweka, maana yake tungepata shilingi trilioni 4.7 kwa mwaka jana, sawasawa na asilimia kumi ya mwaka huu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini haya yanatokea hivyo? Haya ni masuala ambayo Serikali/Wizara ya Fedha lazima myafikirie kwa kina. Vilevile Msajili wa Hazina aangalie kuna mashirika ya hovyo, ni mzigo kwa Serikali, hata ukiyapima kwa huduma, huduma yake haitapimika na hata ukiya-grade ukayalea kama unavyoilea ATCL yatatutia hasara mpaka Yesu anarudi na faida inayotokana kwa third party hutaweza kuipata. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe Serikali kupitia kwa Msajili wa Hazina, ndani ya Kamati tumetoa mapendekezo kwenye mashirika ya hovyo, ambayo yana mikataba ya hovyo, ambayo yana watendaji ambao hawana weledi, unakuwa na CEO, Wenyeviti wa Bodi na Board of Directors hawana idea hata moja…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)