Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. Janet Zebedayo Mbene

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ileje

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. JANETH Z. MBENE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi nami kuchangia. Naomba kwanza kuwapongeza sana Wenyeviti waliowasilisha ripoti za Kamati zao. Kwa kweli, nasikitika kuwa, muda hautatosha sana kwa sisi kuchangia kikamilifu, lakini nitajitahidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna hoja zinazotolewa na Waheshimiwa Wabunge kuhusiana na kuwa nchi yetu ina rasilimali nyingi sana, lakini bado tuko maskini, kwamba mazao yetu yanauzwa nchi za jirani. Labda kwa ufupi tu niseme kuwa na rasilimali za kutosha peke yake si sababu ya kuwa tajiri, ila tunachotakiwa kufanya ni jinsi gani tunakuwa na taasisi zitakazoweza kugeuza kwa tija rasilimali hizi na kuzifanya kuwa mali, mapato na bidhaa zitakazoendesha uchumi wa nchi, lakini suala la mazao yetu kuuzwa Kenya, Rwanda, Burundi au Uganda vile vile sio tatizo; sisi issue kwetu ni kuwa tunapata mapato kutokana na biashara hiyo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza sisi tuko kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa vyovyote vile itafika siku ambayo mazao, watu, bidhaa vitakuwa vinapita kama vile vinatoka hapa kwenda Morogoro. Kwa hiyo hilo lisiwe ni jambo la kuchukua muda mwingi kulizungumza,
tunachotaka kuona hapa ni kuwa mazao yetu au bidhaa zinazokwenda nchi nyingine yanasimamiwa vizuri, kwa maana ya bei nzuri na mapato yanayoingia katika Taifa letu, lakini vile vile na nchi yetu pia inaruhusiwa kuingiza mazao kutoka nchi nyingine za jirani kupitia kwetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna suala la magogo yanayotoka Congo na Zambia. Hakuna ubaya wowote magogo yale yakapitishwa Tanzania na sisi tukaya-export kama vile na sisi mali zetu zinavyokuwa exported na nchi jirani kwa sababu, mwisho wa yote ni biashara ya kimataifa. Kwa hiyo, nataka kuihamasisha Serikali, kama vile ambavyo sisi mazao yetu yanaenda kuuzwa nchi nyingine, basi na ya nchi nyingine yapitie kwetu, ili na sisi tuweze kuoata mapato yanayotokana na usafirishaji wa mazao hayo and afterall sisi ni hub kutokana na location yetu ya kijiografia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningependa vile vile kuzungumzia kwa kifupi sana suala la mashirika ya umma. Kwa kweli, mimi bado nina imani kubwa kuwa mashirika ya umma mengi ni mzigo kwa Taifa letu, kwa sababu, ni muda mrefu sana yanaendeshwa kwa hasara. Ingekuwa ni kampuni binafsi miaka mitatu, minne, mitano, inatosha kuonesha kuwa hili shirika halifai. Kwa hiyo, ninachotaka kusema aidha, tuweke menejimenti ambayo itayageuza haya mashirika yakaendeshwa kibiashara na kiushindani au tuyafunge kwa sababu, yanaendelea kutunyonya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile tuhakikihe kuwa watu tunaowaweka pale, wanawekwa pale kwa ushindani wa uwezo wao na sio wa kuteuliwa. Hili, jambo nafikiri limeshazungumzwa sana humu ndani; ukimweka mtu kwa kumteuwa inakuwa vigumu hata kumdhibiti, lakini ukimwajiri mtu kwa vigezo unampima kwa vigezo vyake vya delivery, akishindwa ku-deliver unamwondoa. Kwa hiyo, kwa kweli, nafikiri kwenye masuala ya Mashirika ya Umma hata tungelipa hayo madeni sidhani kama tutakuwa tumetatua tatizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakuja kwenye suala la msingi ambalo nataka kulichangia leo, ni kuhusiana na kilimo. Bado kilimo ni fursa kubwa sana kwa Watanzania kujiondoa katika umaskini. Ningependa sana kuona Serikali sasa inakuja na mkakati badala ya kila siku kutuambia changamoto, tunazifahamu changamoto zote zilizoko kwenye sekta ya kilimo. Tunaomba sasa tupate mkakati wa Serikali, kwamba je, mnapanga kufanya nini, ili kilimo kiinuke? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kuwa tayari kuna mikakati kwenye mazao. Mazao muhimu ya kibiashara au ambayo tunapeleka nje yana bodi zake na vilevile Serikali imejitahidi sana kuondoa tozo zile ambazo zilikuwa sumbufu. Hata hivyo bado tunataka kuona jinsi gani sasa bodi hizi zinafanya kazi ya kuhakikisha kuwa, wakulima wanawezeshwa kulima kwa tija na wanapata mapato stahili na mwisho wa yote uchumi unakuwa na asilimia kubwa zaidi ya pato letu la Taifa linachangiwa na kilimo ambacho kina watu zaidi ya asilimia 70 ambao wanakitumikia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kutoa pongezi kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu kwa tamko lake la hivi juzi, kuwa sasa hivi wakulima waweze kuuza mazao yao wao wenyewe bila kupitia madalali. Hata hivyo, hata kwa hivyo vyama vya ushirika vya mikoa au vya wilaya lazima watendaji wawe wenye weledi, wenye kujua kuendesha shughuli hizo kibiashara na wawe wazalendo. Kwa hiyo turudi kule kule, tuajiri watu ambao wana uwezo wa kuendesha vyama hivi vya ushirika la sivyo tutarudi, tutakuwa tuna-recycle watu tunaita majina haya tunarudi huku. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile nataka kutoa pongezi sana kwa Mfuko wa Kahawa kwa jinsi ambavyo wamejitahidi kupunguza gharama za tozo. Hata hivyo bado tuna shida kubwa sana ya tozo nyingine ambazo zinatakiwa kuondolewa, ili ziwaguse wakulima moja kwa moja. Tozo nyingi zilizoondolewa kwa mtazamo wangu zinaenda kuwasaidia zaidi wasindikaji, lakini je, wasindikaji wa mazao mengine ni akina nani?

Mheshimiwa Mwenyekiti, wasindikaji kwenye mazao mengine ni haohao wakulima, kwa hiyo unakuwa hujamsaidia sana, lakini kuna tozo ambazo zinaenda kugusa uzalishaji moja kwa moja. Ningependa Serikali iziangalie na hizo iziondoe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka kukimbia haraka haraka kwa sababu ya muda. Kuna suala la korosho, zao la korosho limeonesha kabisa kuwa ni zao ambalo sasa hivi linafanya vizuri sana. Linafanya vizuri sana kwa sababu limewekewa mkazo na Serikali yenyewe, lakini vile vile na bodi yake. Nashangaa kusikia mtu hapa anasema eti zao la korosho halijasaidiwa chochote na Serikali, sijui huyu mwenzetu yeye yuko wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, zao la korosho limewekewa mikakati mizuri, linasimamiwa vizuri na sasa hivi linaenda vizuri. Pamoja na hayo kuna suala la kuhakikisha kuwa wazalishaji wapya wa korosho wanawezeshwa, wazalishaji wapya wa korosho wanapewa pembejeo… (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)