Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

Hon. David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017, Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2017

MHE. DAVID E. SILINDE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nashukuru sana kwa kupata fursa hii ya kujadili hizi report zetu zote tatu, lakini zaidi nitajikita kwenye masuala ya uchumi, hususan kwenye Kamati yetu ya Bajeti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na report kuandikwa na kuelezwa ndani ya Bunge; pamoja na majibu ya Serikali kwa kipindi cha huu mwaka uliopita 2017, kwamba hali ya uchumi ni nzuri, lakini ukipitia kwenye records na taarifa mbalimbali ambazo zimekuwa zikitoka; kwa mfano, kwenye Taarifa ya Easy of Doing Business kwa maana ya wepesi wa kufanya biashara, kwenye viashiria 11 ambavyo vimetoka nchi yetu imeporomoka kwa viashiria saba, yaani kwamba, kila mwaka tumekuwa tukiporomoka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitajikita kwenye kiashiria kimoja tu, upitishaji shehena bandarini na usafirishaji wa bidhaa. Sasa hivi tuko nchi ya 182 kati ya nchi 190 na bandari ndiyo sehemu pekee katika nchi hii ambayo inatuongezea mapato mengi. Asilimia 40 ya mapato ya nchi hii yanapatikana bandarini, lakini hali ilivyo mpaka sasa hivi hali ni mbaya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi ukienda pale bandarini makontena mengi yamezuiwa pale kwa sababu ya contradictions ambazo ziko pale. Watu wa TBS wanasema hawawezi kutoa vibali vya kuruhusu makontena yatoke mpaka wapate certification kutoka TRA. Watu wa TRA hawawezi kuwaruhusu watu kutoa makontena mpaka wapate certification kutoka TBS, unashindwa kujua contradictions za kimamlaka ya watu wawili wanaofanya kazi kwenye Serikali moja zinavyosababisha wananchi waweze kuumia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo mnajikuta kuna masuala ya storage mle ndani, ambayo ni non statutory fee ambayo mtu yeyote angeweza kuachiwa akafanya biashara, lakini leo imekuwa Serikali kama kuwakwamisha wafanyabiashara, ili walipe storage fee, ili kuongeza mapato ambayo yamekuwa yakiendelea. Kwa hiyo ni vizuri Serikali ikaja ikatueleza mikakati na namna ambavyo inaweza kukabiliana na hili jambo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo la pili, kutokana na muda najitahidi kukimbia kimbia. Jambo la pili, ukipitia Taarifa ya IMF na World Bank ambayo wameitoa mwisho wa mwaka, taarifa inatueleza kabisa kwamba, ukipitia Sera yetu ya Kifedha kwa maana ya Monetary Policy pamoja na Fiscal Policy, hizi sera moja inamtafuna mwingine. Kwamba, benki unajikuta kama sasa hivi Benki Kuu inajitahidi kushusha riba, ili mabenki yapate fedha yaweze kukopesha wananchi, lakini ukweli wananchi wanashindwa kukopa pamoja na Benki Kuu kupunguza riba kule ndani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, maana yake ni nini; kwa sababu, ukija kwenye Fiscal Policy ndio Sera ambayo inakula. Yaani kodi ni nyingi kwa maana mtu anashindwa kukopa kwa sababu, anajua nikikopa nitashindwa kulipa, kwa hiyo, inabidi kuangalia hapa je, tunatengeneza uchumi wa namna gani katika hili Taifa na ukiangalia kama sasa hivi tangu Taarifa ya Benki ya Dunia imetolewa, sisi kama Taifa tumeshindwa kutoa maelezo ya kutosha ambayo yanaweza kulisaidia Taifa namna gani ambavyo tunaweza kukabiliana na hii hali ya ukwasi kupungua zaidi hapa nchini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuonesha uchumi kwamba umeendelea kuyumba; ukiangalia sasa hivi Serikali imefunga mabenki, inajitetea yale mabenki wigo wake ni mdogo, lakini ukweli ni kwamba, ukiangalia zile community bank 12, benki karibu nane zinatakiwa zifungwe kwa sababu na zenyewe bado zina-run under profit, kila mwaka zinapata negative ukiangalia kwenye report ambazo wao wenyewe wamezitoa. Kwa hiyo, napenda na jambo hilo vile vile Serikali iweze kukaa na kuliangalia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la ukwasi kupungua; sasa hivi mzunguko wa fedha nchini umepungua kwa zaidi ya asilimia 45. Watu hawawezi kuagiza nje ya nchi na sisi wenyewe tumekuwa tukiiona hiyo hali, lakini bado Serikali imekuwa ikijinasibu kabisa kwamba, fedha zipo zinatosha, lakini hali ya uchumi wa nchi yetu bado umeendelea kuyumba kwa kiwango cha juu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa zimeendelea kuonesha kwamba, ili sera na uchumi uwepo bado ufisadi ndani ya nchi yetu umeendelea kuwepo. Jana Mheshimiwa Heche alijaribu kuzungumzia kidogo tu kuhusu Mradi wa Passport Nchini. Mradi ule umekuwa inflated kwa 40 million US Dollar. Nina taarifa ambazo tumezipata, ni kwamba ule mradi thamani yake halisi ulikuwa ni dola milioni 16, sawasawa na paundi milioni 11, lakini umekuwa inflated to dollar karibu milioni 58, forty million plus.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna taarifa hizi, kuna kampuni ambayo ilishakuwa imepewa Memorandum of Understanding ambayo walipewa vile vile mkataba ambao haukusainiwa mpaka dakika ya mwisho, lakini mwisho wa siku waliingia kampuni mpya ambayo inaitwa ya HID. Hii Kampuni ya HID ambayo ndiyo imefanya hii kazi haijawahi kufanya mradi wa Passport duniani mahali popote. Ni kampuni ambayo kazi yake ni moja tu, inatengeneza hizi security doors, yaani zile kazi ambazo za ku-swap. Sasa ndio kampuni ambayo imeingilia hiyo kazi na ndio imefanya. Imeingia ubia na watu ambao walikuwa NIDA katika kile kipindi ambacho kimepita. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ufisadi bado upo na uchumi umeendelea kuyumba, lakini watu wamekuwa wakifichaficha tu kwa namna fulani. Tuna documents zote kama ambavyo watu wakihitaji sisi tutazikabidhi. Kwa hiyo, tungependa vilevile tunapojadili Sera ya Uchumi na haya mambo lazima vilevile yaweze kujadiliwa, kama tunapinga ufisadi lazima hatua ichukuliwe. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nami naamini kabisa sisi humu ni Wanasiasa na tunaweza hata tukawa ni Mawaziri, tunaweza tukawa hatulijui hili, lakini taarifa za ndani tulizonazo ni juu ya hili jambo kuna ufisadi wa kutisha kwenye mradi wa passport za hapa nchini. Kwa hiyo, ni jambo ambalo linahitaji lipatiwe ufafanuzi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ambalo ningependa kulizungumzia hapa ni kuhusiana na transfer pricing. Nchi yetu pamoja na kwamba, tumekuwa tukipambana kuwakamata wananchi wa kawaida walipe kodi, lakini ukweli ni kwamba, makampuni makubwa yamekuwa yakikwepa kodi katika namna ambayo Serikali haiwezi kupambana nayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nami hili nataka Wizara ya Fedha ijaribu kwenda kuangalia zile regulations (kanuni) zao kuhusiana na haya makampuni makubwa kwenye issue nzima ya transfer of pricing. Nilitoa mfano mmoja, wakati tunapitia kwenye moja ya Kamati, kwa mfano, kampuni ya Petra Diamond, ambayo inafanya kazi ya uchimbaji wa almasi, yenyewe…(Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa mzungumzaji)