Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa hii na mimi nichangie kwenye hoja hii ya Mheshimiwa Waziri wa Fedha na Mipango, Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango. Kwanza, nianze kwa kuiunga mkono hoja hii, lakini pili kwa kumpongeza yeye mwenyewe binafasi na Naibu wake kwa kuleta mpango huu mzuri ambao unatoa dira ya namna ambavyo Serikali itatekeleza majukumu yake kwenye mwaka unaokuja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu, naomba nitoe ufafanuzi kwenye maeneo machache ambayo yamegusa sekta ya maliasili na utalii kwa ujumla wake. Lakini kabla ya kufanya hivyo, nitumie nafasi hii kuwashukuru viongozi wetu wa juu wa Serikali kwa miongozo mbalimbali na maagizo ambayo wamekuwa wakitupa toka wametupa dhamana ya kusimamia sekta hii. Mimi naomba niwape uhakika tu wao pamoja na wananchi wa nchi yetu kwamba sintowaangusha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo ambalo nimeona limejitokeza kwa kiasi kikubwa na ambalo ninaomba nianze kwa kulitolea ufafanuzi kabla sijafika mbali ni suala la kwamba Waziri mpya wa Maliasili na Utalii ameanza kazi kwa kufukua makaburi. Naomba niseme tu kwamba mimi siyo mashuhuri sana kwa ufukuaji wa makaburi, lakini ukiwa Waziri halafu ukawekwa kwenye Wizara ambayo wiki ya kwanza tu hata kabla hujaanza kazi kila mtu anasema umekalia kuti kavu, ni lazima kabla hujaanza kufanya kazi uliyopewa uanze kwanza kwa kusafisha nyumba yako. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa msingi huo, tumeanza kazi ya hygiene kwenye Wizara hii na kazi hii haitakoma mpaka pale ambapo mitandao yote ya watu ambao wako ndani ya Wizara hii wanashiriki kwenye vitendo vya ujangili, wanashiriki kwenye hujuma na wamekuwa wakitajwatajwa kwenye kashfa mbalimbali za rushwa, tutashughulika nao kwanza. Tukimaliza kuing’oa hii mitandao sasa tutaanza kazi kubwa na pana na ya maana zaidi kwa nchi yetu ya kuendelea kuongeza idadi ya watalii, lakini pia kuongeza idadi ya vivutio, pia kuendelea na kazi ya uhifadhi wa rasilimali hii adimu tuliyonayo kwenye nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tutafanya hivyo kwa kuwekeza kwenye kanda nyingine kama Kanda ya Kusini kwa maana ya diversification ambapo kwa sasa tutaelekeza nguvu zetu huko ili kuifungua corridor ya Kusini kiutalii. Serikali imepata fedha, shilingi bilioni takribani juu kidogo ya 300 kwa ajili ya kutekeleza mradi mkubwa wa kuifungua Kanda ya Kusini kiutalii na ninaomba hapa nitambue mchango mkubwa wa Waziri wa Fedha na Mipango, Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango na timu yake, kwa kazi kubwa waliyofanya ya kuandika andiko la mradi huu na hatimaye kufanikisha zoezi la kupata fedha hizi zaidi ya bilioni 300 kwa ajili ya kufungua corridor mpya ya Kusini kitalii na ninaona kwa kweli yuko busy kutekeleza mpango wake ule uliopita na sisi tunamshukuru. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla hatujafika kuanza kutekeleza hii mipango yote mizuri, nilisema ni lazima tuanze kusafisha. Katika kusafisha naomba niseme sikusudii kufukua makaburi ya Mawaziri wazuri waliopita hapo wakapata ajali mbalimbali za kisiasa kama akina Mheshimiwa Maige, Mheshimiwa Kagasheki na Mheshimiwa Maghembe.

Mheshimiwa Mwenyekiti, labda nianze kwa kuzungumzia Waziri mmoja ambaye wenzetu hawa wa Upinzani walimsema sana alipokuwa Waziri wa Maliasili na Utalii na huyu si mwingine ni Mheshimiwa Lazaro Nyalandu. Ninataka niseme tu kwamba rafiki yangu, Mheshimiwa Nassari alizungumza kwa mwembewe nyingi sana hapa Bungeni kwamba kama Dkt. Slaa…

(Hapa baadhi ya Wabunge walizungumza bila kufuata utaratibu)

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Unajua ukiwa unaishi kwenye nyumba ya vioo, usianzishe vita ya mawe, kuna wengine kwa wale mliokuja wapya humu Bungeni mnatakiwa mjifunze mazingira ya humu ndani, kuna watu wanaguswa na kuna watu hawaguswi. Mimi ni katika watu wasioguswa na huwa sipendi mambo ya kipuuzi kabisa hata siku moja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mtu amesema nimeanza kazi kwa kuanza kufukua makaburi sasa sitaki kuwakumbusha yaliyotokea huko nyuma lakini naomba tu niwape uhakika kwamba mimi huwa sichezewi chezewi. Mtu aliyesema nimeanza kazi hii kwa kufukua makaburi na mimi nasema leo nafukua moja na ninaanza kufukua hilo moja kwa maelezo yaliyotolewa na Wabunge hawa wa Upinzani kwenye Bunge lililopita. Walisema Mheshimiwa Lazaro Nyalandu kazi yake ni kustarehe kwenye mahoteli ya kitalii, kazi yake ni kutembea nchi za mbali huko Marekani wapi na warembo, wakasema alitembea alienda Marekani na Aunty Ezekiel.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakasema Ndugu Lazaro Nyalandu anatumia helikopta za wawaekezaji kwa shughuli zake binafsi za kisiasa na Mheshimiwa Nassari alisema kwamba kama yeye kama Dkt. Slaa angeshinda Urais mwaka 2015 na akampa yeye Uwaziri wa Mambo ya Ndani kwa siku moja tu, angeanza kwa kushughulika na Mawaziri wa hovyo kama Mheshimiwa Lazaro Nyalandu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa leo ninaeleza kwamba kwa nini Mheshimiwa Nassari alikuwa sahihi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Nassari alikuwa sahihi kwa sababu wakati Waziri Nyalandu akistarehe kwenye Hoteli ya Serena pale Dar es Salaam akitumia helikopta ya mwekezaji wa TGTS, mezani kwake…….

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, nilichokuwa nataka kusema ni tu kwamba wakati Mheshimiwa Nyalandu Nyalandu akivinjari kwenye Hoteli ya Serena ambapo alikuwa akifanyia kazi zake za Waziri wa Maliasili na Utalii kwenye hoteli ile na akapewa chumba akawa anaishi pale kwa muda wote ule, mezani kwake kulikuwa kuna GN yaani tamko la Serikali kuhusiana na kitu kinachoitwa concession fees kwenye mahoteli ambayo yako ndani ya mbuga ya Serengeti.

KUHUSU UTARATIBU . . .

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Bobali mimi mzoefu humu ndani, wewe unadhani mimi najibu hoja, mimi sijibu hoja mimi nachangia, mwenye hoja yuko pale Waziri wa Fedha na Mipango. Muwe mnajifunza nishasema mimi huwa sichezewi chezewi. Kwa sababu najua Kanuni.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niendelee kuchangia, ninachokisema ni kwamba wakati Mheshimiwa Nyalandu akifanya yote hayo kulikuwa kuna mambo makubwa mawili ambayo napenda tu kuyatolea mfano hapa.

Moja; mezani kwake kama Waziri wa Maliasili na Utalii kulikuwa kuna concession fees ambayo ilikuwa imependekezwa na TANAPA na gazeti likatengenezwa likisubiri signature ya Waziri ili Serikali ianze ku-charge concession fees kwenye mahoteli ya kitalii. Hilo lingeongeza mapato na kwa mwaka huo wa 2014 tungeweza kukusanya bilioni 16 lakini Waziri yule hakusaini hiyo GN mpaka anaondoka madarakani, maana yake Mheshimiwa Nyalandu aliikosesha Serikali mapato ya takribani bilioni 32, hilo ni moja na ni jambo ambalo watu wa mahoteli walipinga na baada ya watu wa mahoteli kupinga, Serikali ikashitakiwa Mahakamani, Serikali ikapata ushindi mahakamani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo, Waziri alikuwa hana lolote lile la kuamua kwa sababu kuna amri ya Mahakama kwamba Serikali iko sahihi na i-charge concession fees, lakini Waziri yule hakusaini kwa miaka miwili mpaka anatoka madarakani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mambo kama haya ukiniambia nafukua makaburi mniache tu niendelee kufukua lazima nifukue kwa sababu bila kuweka mambo sawa, bila kujua kwa nini Mheshimiwa Nyalandu hakusaini, bila kujua Mheshimiwa Nyalandu alikuwa anashirikiana na akina nani na je, alikuwa anashirikiana nao wapo ama wameondoka? Huwezi kufanya kazi yako vizuri. Ndiyo maana hata Mawaziri watakaowekwa pale wataendelea kutolewa tu, wataendelea kukalia kuti kavu tu, sasa mimi siko tayari kukalia kuti kavu, hata nikikaa miezi mitatu nitakuwa nimeinyoosha hii sekta. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili napenda kuzungumzia mahusiano ya kutatanisha aliyokuwa nayo Waziri wa Maliasili na Utalii Ndugu Nyalandu na wawekezaji wa taasisi maarufu inajulikana kama Friedkin Family Foundation ni billionea kutoka nchi ya Marekani ambayo ilikuwa ina Makampuni yanayofanya kazi mbalimbali za utalii hapa na bado yapo mpaka sasa. Moja inaitwa Mwiba Holdings, nyingine inaitwa Winged to Winrose na nyingine inaitwa Tanzania Game Trackers Safaris. Kampuni zote hizi, Kampuni ya TGTS ilipewa vitalu zaidi ya vitano ambazo ingepaswa kupewa kwa mujibu wa sheria maana yake ni kwmba hapo kuna mazingira ya kutatanisha, kuna mambo hayako sawa na bado Kampuni hii ipo na inafanya kazi kwenye sekta hii, ukisema nisifufue makaburi utakuwa unanionea, ni lazima nijue kwa nini waliopewa vitalu zaidi ya vitano? Kwa nini wanaendelea kuwinda?

Kampuni ya Mwiba Holdings ina tuhuma za ujangili kwamba Kampuni inawinda, inafaya kazi za utalii lakini imekamatwa na nyara za Serikali na hizi Kampuni zote zinamilikiwa na mtu mmoja anaiywa Tom Friedkin ambaye ni rafiki wa Ndugu Nyalandu na Waziri huyu kama nilivyosema huko nyuma alikuwa akifanya kampeni za Urais kipindi kile tulijaribu na sisi kuomba ridhaa ya Chama kugombea Urais, alikuwa akifanya kampeni zake, akizunguka na helkopta ambayo inamilikiwa na Kampuni ya huyu Ndugu Tom Friedkin. Sasa katika mazingira kama hayo, Waziri wa Maliasili na Utalii, GN ya kusaini kuhusu kudai concession fee iko mezani kwao hausaini na unaka kwenye hoteli...

T A A R I F A . . .

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, zama zinabadilika na uongozi pia unabadilika. Kwenye Wizara ya Maliasili na Utalii sasa hivi kuna Waziri ambaye anaweza kumchukulia hatua Ndugu Nyalandu, kwa hivyo kama ndiyo kilio chako Ndugu Haonga mimi nitaagiza hapa TAKUKURU pamoja na Jeshi la Polisi wayasikilize haya ninayosema, wachukue Hansard, wakafanye uchunguzi ili waweze kumchukulia hatua Ndugu Nyalandu wala hilo halisumbui. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ndiyo kiu yako na wewe kama mwananchi na kama Mbunge kwamba kwa nini Nyalandu hajafika mahakamani, mahakama bado zipo na jinai haiishi muda, jinai hata miaka 100 ipo tu, kwa hiyo vyombo vinavyohusika vichukue hatua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo Ndugu Nyalandu alikuwa akitumia helicopter za Kampuni za huyu Ndugu Tom Friedkin kufanya kampeni zake za Urais lakini pia kufanya kampeni zake za ubunge Jimboni. Katika mazingira kama hayo, dada yangu Devotha Minja ukisema nisifukue makaburi utakuwa unanionea bure tu. Mniache nifukue haya makaburi, tuweke sawa nchi, tumsaidie Mheshimiwa Rais ndiyo kazi tuliyopewa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la tatu, vitalu vya uwindaji kabla ya Ndugu Nyalandu vilikuwa vikitolewa kwa makampuni mbalimbali na muda wa kuwinda ulikuwa ni katika kipindi cha miezi mitatu tu, kati ya Julai mpaka Oktoba ili kuwapa nafasi wale wanyama kupumua na pia kuzaliana, lakini...

T A A R I F A . . .

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naendelea na mchango wangu, Ndugu Nyalandu alivyopewa tu kiti cha Waziri wa Maliasili na Utalii alichokifanya bila huruma yoyote ile, bila uzalendo wowote ule alianzisha mchakato wa kubadilisha...

MWENYEKITI: Ahsante.