Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Zainab Athuman Katimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. ZAINAB A. KATIMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye sekta ya nishati, Mpango unaonesha mpaka mwaka 2020 uzalishaji wa umeme ufikie zaidi ya Mw 5000 Installed Capacity, kwa sasa ni Mw 1358 na mradi wa Stieglers Gorge utazalisha Mw 2100. Je, Mw 1542 itatokana na mradi upi ili kufikia lengo la Mw 5000 mpaka ifikapo mwaka 2020?

Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango haujaainisha kama itashirikisha sekta binafsi au itatumia mradi upi kufikia lengo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali katika mradi wa Stieglers Gorge itumie teknolojia ya kisasa ya electricity generation by recycling of water ili kuepusha kusuasua kwa uzalishaji wa umeme kutokana na upungufu wa kina cha maji kwenye vyanzo vya maji. Mfano wa teknolojia iliyotumika kwenye The Grand Ethiopian Renaissance Dam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukurasa namba 14 umeonesha projection ya population growth. Tanzania katika miaka michache ijayo itakuwa na idadi kubwa ya watu. Je, tumejiandaa katika mipango yetu kuhakikisha kuwa ongezeko hili la watu sio tegemezi na lisiwe mzigo wa Serikali?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kilimo ndiyo uti wa mgongo wa uchumi wa Mtanzania. Je, Serikali imeandaa mikakati gani ya kuimarisha mazingira ya Agro Business Tanzania? Kwa mfano, kuna vyombo kama Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko ambayo ni chombo cha kusaidia wakulima wanapata soko la uhakika wa mazao yao, lakini Bodi hii haijawezeshwa kibajeti kutimiza malengo. Mfano, mwingine ni Benki ya Maendeleo ya Kilimo ambayo inachangamoto ya mtaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naishauri Serikali iweke katika mipango yake namna ya kuwezesha vyombo vilivyo vya kuendeleza kilimo Tanzania. Lakini Serikali iweke mipango ya makusudi ya kuwahakikishia wakulima soko la mazao yao ili kilimo kiweze kuleta tija. Pia itoe kibali kwa Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko kupata shilingi bilioni 8.9 loan kutoka NSSF na kibali cha kupata mkopo wa bilioni 6 kutoka Azania Bank ili Bodi ifanye kazi zake kwa mujibu wa sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imefikia wapi katika kuleta Muswada wa sheria itakayoanzisha Price Stabilazation Fund, mfuko utakaoweza kuwa suluhisho la kumlinda mkulima pale bei za mazao zinapoanguka, kwa mfano mbaazi mwaka huu?