Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Suzana Chogisasi Mgonukulima

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. SUZANA C. MGONOKULIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Tanzania inataka iwe nchi ya viwanda, tuboreshe sekta ya kilimo kwa kuhakikisha kwamba mikopo kwa wakulima inapatikana. Tukifanya hivyo tutakuwa tumewawezesha wakulima kulima kilimo bora. Kilimo bora kinatokana na wakulima kuwa na mbegu bora na mbolea kwa wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu sera ya elimu bure, ni miaka miwili kama Taifa tumeona kuwa elimu bure inaathari kutokana na kuporomoka kwa ufaulu wa wanafunzi. Katika mpango huu uliopendekezwa na Waziri wa Fedha, je,kuna mkakati wa makusudi wa kutatua matatizo yanayoikabili sekta ya elimu? Elimu ya kutosha inatakiwa kutolewa kwa wananchi wajue kuna baadhi ya shughuli za elimu kama wananchi wanapaswa kuchangia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mpango huu uliopendekezwa kwa mwaka 2018/2019, hakuna sehemu iliyoonesha ukuzaji wa viwanda katika Mkoa wa Iringa ambavyo vilikuwepo katika Mkoa huo. Mkoa wa Iringa miaka ya nyuma ulikuwa na viwanda vya COTEX, Cocacola, IMAC, SIDO na Tyre,viwanda hivi viliwasaidia sana wananchi wa Mkoa wa Iringa na maeneo mengine ndani ya nchi yetu kupata ajira, lakini katika mpango uliopendekezwa sijaona sehemu yoyote inayoonesha kwa mwaka 2018/2019 kuhakikisha viwanda hivyo vinaimarishwa ili kupatia ajira wananchi wa Mkoa wa Iringa na maeneo mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba suala hili lipewe kipaumbele.