Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Omar Abdallah Kigoda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. OMARI A. KIGODA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa nianze kwa kuipongeza Serikali kwa juhudi zake katika kuleta maendeleo katika nchi yetu, bila ya kusahau kumpa pongezi kubwa sana Rais wetu, Mheshimiwa John P. Magufuli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mipango endelevu inahitaji kwanza kabisa kutokuwa na watu wajinga, maradhi na maskini. Lazima mipango hii iendane na kuwanyanyua watu na kuwasaidia katika utendaji wao wa kulinyanyua Taifa. Serikali ihakikishe huduma ya ukusanyaji kodi kwa kutumia mashine za kielektroniki inakuwepo nchi nzima. Hii itasaidia ukusanyaji wa haraka na kutopoteza muda wa kutoa kodi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine ni lazima Serikali ihakikishe huduma za jamii kama maji, umeme na mengineyo zinapatikana kwa wingi ili muda mwingi watu tuutumie kwenye kujenga nchi yetu. Maendeleo ya nchi lazima tuwe na manpower ya kutosha, kwa hiyo, tukihakikisha huduma za jamii zipo itasaidia kuwa na manpower ya kutosha kujenga uchumi wa nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali lazima ihakikishe inazingatia suala la afya ya kila mwananchi inakaa sawa na inatibika kwa urahisi, ili kutokuwa na Taifa la wenye maradhi; hii itadhoofisha ukuaji wa uchumi wetu wetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kingine ni suala la amani. Lazima nchi iwe na amani, ili kila mtu awe huru katika kutekeleza kazi zake za kulijenga Taifa. Lazima Serikali isisitize watu kufanya kazi ili tuweze kukwamuka kutoka tulipo, twende mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, infrastructures zetu lazima tuhakikishe zinatumika na lazima tuweke mazingira mazuri kwa watumiaji. Mfano, gesi lazima itumike kwenye viwanda vyetu ili kuwa na uzalishaji wa kutosha. Lazima barabara zetu ziwe za kupitika muda wote, hii itasaidia kwa wakulima na wafugaji hata waoa huduma kufika kwenye point haraka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la elimu ni muhimu sana. Taifa la wajinga haliwezi kuwa na maendeleo au kujikwamua kiuchumi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na jiografia ya nchi yetu kuna infrastructures ambazo ni za mkakati especially kiuchumi, kwa mfano, barabara ya Handeni – Mziha – Dumila na nyingine nyingi. Hizi infrastructures lazima tuzitengeneze ili ziweze kutumika katika mzunguko wa biashara kwenye nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hakuna Taifa lililoendelea bila kuwahusisha wafanyabiashara wakubwa, pia na kuwahusisha katika uwekezaji. Hivyo, ni lazima Serikali iwe karibu na wafanyabiashara na kusikia matatizo yao na kujadiliana ili kuweka mambo sawa.

Mhershimiwa Mwenyekiti, miaka 30 iliyopita South Korea tulikuwanao almost sawa, lakini kwa sasa wamepiga hatua sana kimaendeleo. Walichofanya ni kuhakikisha wanaweka mazingira mazuri ya uwekezaji na Serikali ilibaki kuchukua kodi kutokana na uwekezaji huo, pia kuhakikisha hiyo kodi inatumika ipasavyo kwenye huduma za jamii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho napenda kumshauri Waziri, hii mipango tunayopanga ni mizuri tu endapo utekelezaji wake utapewa kipaumbele na msisitizo wa kila mtu katika sekta yake lazima afanye kazi. Hakuna uchumi unaopanda kwenye Taifa la wavivu, lazima msisitizo wa uwajibikaji usemwe mara kwa mara.