Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, na mimi nikushukuru jioni ya leo kwa kunipa nafasi niweze kuzungumzia juu ya Mpango wa Maendeleo wa mwaka 2018/ 2019.

Mheshimiwa Mwenyekiti, yamezungumzwa mengi. Waliozungumza wamezungumza lakini nataka tu niwaambie Waheshimiwa Wabunge wenzangu kwamba ukipitia kitabu hiki mengi ya msingi Mheshimiwa Waziri ameyazungumza ukianzia ukurasa wa 42 mpaka 53 yote ambayo yanayohusu maendeleo ya Tanzania yamezungumzwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nitajikita kwenye vitu vitatu au vinne tu, ni Public Private Partnership. Mheshimiwa Waziri mimi naomba ujikite hapa, tutapunguza matatizo kwa sababu nchi hii ni kubwa, ina changamoto mbalimbali hatuwezi ku-invest kwa kutumia our own funds, lazima tujikite kwenye Public Private Partnership. Mfano mzuri tu ni Daraja la Kigamboni. Tumeona jinsi ambavyo return kubwa inapatikana pale. Kuna usafiri DART, yote hiyo ni mifano mizuri. Mimi naomba usipate kigugumizi Mheshimiwa Waziri, hebu tuone namna gani tunaweza kujikita huko zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ni suala la VETA, naomba mfumo wa VETA ubadilike. Elimu inayotolewa kwenye VETA ni nzuri sana na tunakwenda kwenye nchi ya viwanda, lakini elimu inayotolewa si ya kisasa. Tuone namna ya kuwaandaa vijana wetu tuweze kutoa elimu ambayo itasaidia kupata vijana tuweze kuwaajiri katika viwanda vyetu hivi. Ukizingatia viwanda ni vya kisasa, kwa hiyo vitahitaji vijana ambao wanasoma au wanapata elimu yenye IT base.

Meshimiwa Mwenyekiti, lingine ni suala la viwanda, tunazungumza kufufua viwanda, mimi naamini vile viwanda vya enzi ya Mwalimu Nyerere havifai tena. Viwanda sasa hivi ni teknolojia ya kisasa ni eneo dogo kwa hiyo tujikite kuwa na viwanda vichache lakini ambavyo vitakuwa na tija na nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ambalo ningependa kulizungumzia ni suala la bomba la mafuta ambalo linatokea Uganda hadi Tanga. Nimeona katika Mpango huu mmezungumzia namna ya kuweka miundombinu na moja wapo ya eneo ambalo mmeligusia ni eneo la barabara ambalo linatokea Handeni hadi Singida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme kabisa kwamba mpango huu ni lazima utekelezeke kwa sababu njia hii ukiacha bomba la mafuta linapita, lakini pia litasaidia kuinua uchumi wa mikoa minne ya Tanga, Singida, Dodoma. Nimeona niyazungumzie hapa nikiamini kabisa ni maeneo muhimu ambayo yatasaidia kuinua uchumi wa nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ambalo ningependa kwenda haraka haraka ni eneo la research and development. Watu tunazungumza hapa, yamezungumzwa mengi sana lakini naomba sasa Mheshimiwa Waziri wa Fedha hebu tuwekeze kiasi kikubwa sana kwenye research. Research na development ndiyo ambayo inaweza kututoa hapa kuona kwamba tubebe yapi tuache yapi na tuwe pia na mpango wa muda mfupi na mpango wa muda mrefu. Kwa sabbu mipango ni mingi na yote inatakiwa kutekelezeka lakini tukitumia research and development maana yake tunaweza tukajua kwamba tuwe na priority ipi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe mfano mmoja tu; hata nchi za China na Malaysia, wenzetu viongozi waliotoka huko mbali walitumia wataalam. Hebu nikuombe Dkt. Mpango na Naibu Waziri hebu kaa na timu, kaa na panel ya wachumi uje na mpango mdogo ambao unaweza kututoa hapa Tanzania tulipo na kwenda mbele zaidi. Haya wanayolamimika Waheshimiwa Wabunge ni maeneo ya msingi kabisa na ninaamini mawazo ambayo yanatoka katika maeneo yetu ya uwakilishi yana maana kubwa.

Mimi sipendi kukulaumu lakini naamini kabisa haya ambayo waheshimiwa Wabunge wameyasema yana tija na yana faida kubwa na mimi naomba kupitia wataalam wako, hebu yachukue yafanyie kazi. Ahsante.