Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Jitu Vrajlal Soni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. JITU V. SONI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza naomba nimshukuru Mwenyekiti Mungu kwa kunipa fursa ya kuchangia leo, lakini pia niipongeze Wizara kwa kuleta Mpango, ni Mpango huu wa miaka mitano ambao tunanyofoa vipande vipande kila mwaka ili kuutekeleza mpango huu. Hakuna cha ajabu na hakuna kitu kipya, ni mambo tuliyoyapitisha mwaka wa kwanza tulipoingia Bungeni. Muhimu ni vipaumbele, mimi naona tumepishana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye vipaumbele kuna mambo ambayo tungebadilisha, yale ya kusogea huko mbele na yale ambayo tungeanza nayo. Muhimu kabisa katika mpangio huu, na kitu ambacho sijaona kama kimewekwa katika mpango wa mwaka huu ambao tunataka kuutekeleza, (2018/2019) ni suala la utafiti. Hakuna nchi inayoweza kuendelea bila ya kuwekeza katika utafiti katika Nyanja zote, iwe kilimo, mifugo, uvuvi, elimu, sayansi, afya na masuala mengine yote kwa kweli hata bajeti ambayo huwa tunatenga kwenye utafiti huwa inakuwa ni ndogo sana, haitoshi hata kwa kitengo kimoja. Katika vituo 16 vya utafiti vile vifaa vyote sasa hivi vimekaribia kuwa vimepitwa na wakati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia sehemu nyingine ambayo ingeweza kutusaidia sana ni katika masuala ya hali ya hewa, tungewekeza zaidi huko. Kama tunataka wakulima wetu wanufaike tukiwekeza kwenye masuala ya hali ya hewa, kama ilivyo kwenye nchi za wenzetu unaambiwa kesho mvua itanyesha muda wa saa fulani, hata wakulima wetu, mimi ninaweza kwenda kupanda mbegu leo kwenye udongo wakati mkavu lakini nina uhakika wa mazao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningeomba Serikali ikae pamoja na kuangalia suala zima la uratibu. Hapa kila Wizara inajitegemea kama vile ni Serikali yenyewe; mfanye kazi kama timu. Niwapongeze juzi Mawaziri wannne walipozindua ule mpango wa viwanda kila mkoa na viwanda, huo ndio uratibu inatakiwa mkae mfanye kazi kwa pamoja. Tuna mifano mingi, tumechimba visima leo mwaka wa tatu umeme haujafikishwa, lakini ingekuwa mnafanya kazi kwa kuratibu Wizara zote, idara zote zinafanya kazi kwa pamoja miradi ile ingekuwa inatekelezwa na mafanikio yangekuwa yanaonekana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni suala la kuwa na sera na mfumo wa kodi ambao ni stable, ambao haubadiliki kila wakati. Mwaka huu tunaweza tukapitisha jambo fulani watu wakaona sera imekaa vizuri na masuala ya kodi, tax regime imekaa vizuri mwakani tumebadilisha tunarudisha, hiyo ndiyo inafanya watu warudi nyuma na kwa mfumo huu hatutoweza kuendelea kwenye masuala ya viwanda tunayotarajia kwamba itashika kasi. Ni muhimu viwanda vile vidogo na vidogo kabisa mngevi-regulate; haya mambo ya Osha, fire, nani mngewaondoa mtu akishalipa leseni yake na muanzishe one stop center kila mkoa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwenye sheria mtu asipojua sheria haikupi kinga mahakamani lakini tungekuwa na center moja; mimi nikienda uniambie ni kiasi fulani nikilipa masuala mengine yote wao ndio watanielekeza. Kila mkoa kuwe na one stop center watu wafanye kazi na viwanda vidogo na nini kama mlivyo-regulate kwenye uzalishaji mdogo vivyo hivyo fanyeni kwenye viwanda, pasiwe na urasimu mkubwa utakuwa na mafanikio makubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, muhimu kuliko yote pia ni kuwekeza kwenye Benki ya TADB. Wakulima hawahitaji kupewa sadaka wala ruzuku, wekeni pesa kwenye benki tukakope na si wajanja wajanja. Wakulima wanaweza kukopa, wakafanya shughuli zao wakalipa hizo hela.Hiyo benki leo haina hela. Mkulima wa kati na wa juu kama anashindwa kukopa pale mdogo atapataje? Kwa hiyo, ninaomba tuwekeze pale na tuhakikishe kwamba benki hiyo inakuwa na mtaji wa kutosha.

Mheshimiwa Mawenyekiti, lingine tukirudi kwenye suala la utafiti ni cost of production. Utakuwa na viwanda, lakini kutokana na utitiri wa hizi regulatolly bodies yaani taasisi za udhibiti unakuta tozo zao zinakuwa ni nyingi kiasi ambacho hata tukizalisha gharama ya ile bidhaa yetu siku zote itakuwa juu kuliko bidhaa ambayo unaagiza kutoka nje ya nchi. Leo hii hata mfumo wetu ukiagiza bidhaa kutoka nje nyingi hazina kodi, hasa zinazotoka kwenye nchi za Afrika Mashariki na Kati. Hayo usipoyafanyia kazi hata tukiwa na viwanda hapa bidhaa zetu hazitauzika. Kwa hiyo, ni vizuri ndani ya Wizara ya Fedha na Mipango mfanyie kazi suala la utafiti ili tuweze kupata…(Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)