Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

Hon. Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Taifa unaokusudiwa kutekelezwa na Serikali pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango na Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2018/2019

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili na mimi niweze kuchangia katika Mpango wa Taifa mwaka 2018/2019. Kabla ya hapo kwanza nianze kwa habari ya uwanja wa ndege wa Chato. Mimi binafsi napenda kusema kwamba Chato iko Geita na Geita kuna watu lakini na kanda yote ile kuna watu, kwa hiyo tunahitaji huduma ya kiwanja cha ndege. Kwa hiyo, Serikali haijafanya makosa kujenga kiwanja Chato kutokana na shughuli za kiuchumi zilizopo kule. Sisi Wabunge na wananchi kwa ujumla tunahitaji kuwa na kiwanja tena kikubwa zaidi ya hicho. Kwa hiyo, niombe Serikali iendelee kuwekeza fedha zaidi ili kuwezesha ujenzi wa hicho kiwanja cha Chato kwa sababu kitawezesha wananchi wote wa Geita, Kahama pamoja na sehemu mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, siku za nyuma tulikuwa tunatumia uwanja wa Mwanza. Uwanja wa Mwanza ni mbali na wakati mwingine kuvuka feri pale unaweza ukakuta feri haipo kwa hiyo unaweza ukachelewa hata ndege. Sasa hivi kwa kuwa na kiwanja Chato kinaturahisishia maisha. Na sisi ni Watanzania vilevile kama Watanzania wengine ambao wana viwanja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la ujenzi wa jengo la TRA kule Chato. Mimi nadhani tunatakiwa kujenga vitu vya viwango. Kwa hiyo, mimi niipongeze TRA kwa kujenga jengo zuri katika eneo hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo niende sasa katika Mpango. Nampongeza Mheshimiwa Waziri pamoja na Naibu wake kwa kutuletea Mpango mzuri. Kwa upande wa barabara nilikuwa naangalia jinsi ambavyo wamejikita kuangalia miundominu muhimu kwa ajili ya kuwezesha uchumi wa kati, kulingana na Sera ya Taifa, kwamba tumejipanga kuwa na uchumi wa kati mpaka kufikia mwaka 2025. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu hiyo nilikuwa napenda kupongeza kwa upande wa barabara. Niombe sasa kwamba kwa upande wa barabara ile Sera ya Taifa ya kusema kwamba tutaunganisha kwa barabara za lami mikoa kwa mikoa, lakini vilevile wilaya kwa mkoa. Kwa hiyo, mimi nilikuwa nashauri tuwekeze fedha nyingi kwenye upande huo ili kuweza kuwezesha kuiunganisha mikoa. Kwa mfano kuna hii barabara ya kutoka Geita ambayo inaunganisha Mkoa wa Shinyanga pamoja na Mkoa wa Geita. Barabara kutoka Geita kupitia Bukoli kwenda mpaka Kahama ni barabara muhimu sana kiuchumi. Kwanza ndio barabara inayotumika na magari mengi yanayobeba mizigo mbalimbali kwa ajili ya kupeleka shughuli bidhaa kwenye shughuli za madini katika mgodi wa GGM pamoja na wachimbaji wadogo wadogo. Kwa hiyo, ninaomba barabara hii isisahaulike kwenye mpango ujao ili ianze kujengwa kwa sababu ni barabara ya muda mrefu imekuwa siku nyingi inazungumziwa lakini hatuoni utekelezaji wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile ili tuweze kufikia uchumi wa kati lazima Serikali iwekeze kwenye kilimo. Kwa mfano sehemu ambazo kuna maziwa pamoja na mito tuangalie kilimo cha umwagiliaji. Nikiangalia Getia tumezungukwa na Ziwa Victoria, tuanzishe miradi ya umwagiliaji ili kuwawezesha wananchi kuweza kuwa na vyakula pia kuwa na uwezo wa kupata bidhaa ili ziweze kutumika katika viwanda vyetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu upande wa elimu. Ili tuweze kuwa na Tanzania ya viwanda lazima tuwekeze kwenye elimu. Kikubwa zaidi, kuwianisha na Sera ya Taifa ya kuwa na VETA kila wilaya mkoa. Niombe suala hili Serikali iwekeze kwenye mpango, kwamba kila mkoa tuwe na chuo cha VETA. Kuna wilaya na mikoa mingi ambako hatuna VETA. Kwa kuwa vijana wengi wanahitaji elimu ya VETA kwa hiyo niombe sasa kwenye mipango yetu na bajeti zijazo tuhakikishe fedha zinatengwa kwa ajili ya kujenga VETA katika wilaya na mikoa yote ili kuwawezesha vijana wetu kupata ujuzi mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa hivi tunatarajia kupeleka umeme kwenye kila kijijiā€¦(Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.